Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 27:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Siku hiyo, Akisi akamupa muji wa Ziklagi. Kwa hiyo, tangu siku hiyo muji wa Ziklagi ukakuwa mali ya wafalme wa Yuda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 27:6
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya kufa kwa Saulo, Daudi alirudi kisha kuwashinda Waamaleki, akakaa Ziklagi kwa muda wa siku mbili.


Hawa ndio wanaume ambao walijiunga na Daudi kule Ziklagi, alipokuwa hana uhuru wowote wa kutembea kwa sababu ya mufalme Saulo mwana wa Kisi. Watu hawa walikuwa kati ya waaskari mashujaa waliomusaidia katika vita.


Waaskari wengine wa kabila la Manase, wakatoroka na kwenda kujiunga na Daudi, wakati alipoondoka pamoja na Wafilistini kwenda kupigana na mufalme Saulo. (Lakini hata hivyo, hakuwasaidia maana watawala wa Wafilistini walifanya shauri wamufukuze arudie Ziklagi wakisema: “Tutahatarisa maisha yetu kwa sababu atatutoroka na kurudia kwa bwana wake Saulo.”)


Wengine walikaa katika muji wa Ziklagi, Mekona na vijiji vilivyoizunguka.


Alipomwua yule Mufilistini Goliati, alihatarisha maisha yake, naye Yawe aliwapa Waisraeli ushindi mukubwa. Wewe ulipoona jambo lile ulifurahi. Kwa nini unataka kutenda zambi kwa kumwanga damu isiyokuwa na kosa kwa kumwua Daudi bila sababu?”


Siku moja, Daudi akamwambia Akisi: “Kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ninakuomba unipe muji mumoja katika inchi yako kusudi ukuwe pahali pangu pa kuishi. Hakuna faida kwangu kuishi nawe katika muji huu wa kifalme.”


Lakini wakubwa wa Wafilistini walimukasirikia sana Akisi, wakamwambia: “Umurudishe aende pahali ulipomupa akae. Asiende hata kidogo pamoja nasi kwa vita, kama sivyo wakati wa vita atageuka na kuwa adui yetu. Hauoni kwamba mutu huyu atapata njia nzuri ya kupatana na bwana wake halafu kuwa adui yetu katika vita?


Kisha siku tatu, Daudi na watu wake wakarudi Ziklagi. Waamaleki walikuwa wamekwisha kushambulia Negebu pamoja na muji wa Ziklagi na kuuteketeza kwa moto.


Sisi tulishambulia Negebu ya Wakereti na eneo la Yuda pamoja na Negebu ya Kalebu. Muji wa Ziklagi tuliuteketeza kwa moto.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ