Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 27:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kwa hiyo, mara moja Daudi na watu wake mia sita wakaenda kwa Akisi mwana wa Maoki, mufalme wa Gati.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 27:2
7 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hawa ndio wanaume ambao walijiunga na Daudi kule Ziklagi, alipokuwa hana uhuru wowote wa kutembea kwa sababu ya mufalme Saulo mwana wa Kisi. Watu hawa walikuwa kati ya waaskari mashujaa waliomusaidia katika vita.


Ahimeleki akamujibu: “Upanga wa Goliati Mufilistini uliyemwua kwenye bonde la Ela uko nyuma ya efodi, unafungwa katika kitambaa. Ikiwa unataka kuukamata basi, uukamate maana hakuna upanga mwingine hapa.” Daudi akamwambia: “Hakuna upanga mwingine kama huo; unipe.”


Siku hiyo, Daudi alimukimbia Saulo, akaenda kwa mufalme Akisi wa Gati.


Kwa hiyo Daudi akawaambia watu wake: “Kila mutu apakatie upanga wake kwenye kiuno.” Kila mutu akapakatia upanga wake, na Daudi vilevile akapakatia upanga wake. Watu yapata mia ine wakamufuata Daudi na watu mia mbili wakabaki na mizigo.


Daudi akamwomba Yawe shauri: “Nikifuata kundi hili nitalikamata?” Yawe akamujibu: “Ulifuate maana utalipata na kuwaokoa hao waliotekwa.”


Kwa hiyo, Daudi akaondoka pamoja na wale watu mia sita aliokuwa nao. Walipofika kwenye kijito cha Besori, wakawakuta wamoja kati ya watu waliotekwa wameachwa pale.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ