Hawa ndio wanaume ambao walijiunga na Daudi kule Ziklagi, alipokuwa hana uhuru wowote wa kutembea kwa sababu ya mufalme Saulo mwana wa Kisi. Watu hawa walikuwa kati ya waaskari mashujaa waliomusaidia katika vita.
Ahimeleki akamujibu: “Upanga wa Goliati Mufilistini uliyemwua kwenye bonde la Ela uko nyuma ya efodi, unafungwa katika kitambaa. Ikiwa unataka kuukamata basi, uukamate maana hakuna upanga mwingine hapa.” Daudi akamwambia: “Hakuna upanga mwingine kama huo; unipe.”
Kwa hiyo Daudi akawaambia watu wake: “Kila mutu apakatie upanga wake kwenye kiuno.” Kila mutu akapakatia upanga wake, na Daudi vilevile akapakatia upanga wake. Watu yapata mia ine wakamufuata Daudi na watu mia mbili wakabaki na mizigo.
Kwa hiyo, Daudi akaondoka pamoja na wale watu mia sita aliokuwa nao. Walipofika kwenye kijito cha Besori, wakawakuta wamoja kati ya watu waliotekwa wameachwa pale.