Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 26:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Abisai akamwambia Daudi: “Leo Mungu amemutia adui yako katika mikono yako. Basi, uniache nimushindilie katika udongo kwa pigo moja tu la mukuki. Sitamupiga mara mbili.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 26:8
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, Abisayi mwana wa Zeruya akamwambia mufalme: “Kwa nini huyu anayekuwa sawa imbwa mufu akulaani wewe bwana wangu mufalme? Uniruhusu nimwendee, nami nitakikata kichwa chake.”


Nitashangilia na kufurahia wema wako, maana wewe unaona taabu yangu, unajua huzuni yangu.


Kisha, Yohana mwana wa Karea akazungumuza na Gedalia kwa siri kule Misipa, akamwambia: Uniruhusu niende nimwue Isimaeli mwana wa Netania, na hakuna mutu yeyote atakayejua. Kwa nini kumwachilia yeye akuue na Wayuda wote waliokusanyika hapa watawanyike na Wayuda waliobaki waangamie?


Mbona munafanya mipango juu ya Yawe? Yeye atawakomesha na kuwaangamiza, wala mupinzani wake hataweza kusimama tena.


Maana Mungu amewafanya watu wote kama wafungwa kwa sababu ya kuasi kwao, kusudi awahurumie wote.


Mutu mumoja anaweza namna gani kuwashinda watu elfu moja, au watu wawili wanaweza namna gani kuwashinda watu elfu kumi, isipokuwa kama mulinzi wao amewatupa, Yawe amewaacha?


Yawe akawapa amani kila pahali katika inchi kama vile alivyowaapia wazee wao. Hakuna adui yeyote aliyesubutu kuwashambulia maana Yawe alikuwa amewatia waadui hao katika mikono yao.


Basi watu wa kabila la Yuda wakaenda kufanya mashambulio, naye Yawe akawatia Wakanana na Waperizi katika mikono yao, wakawaua watu elfu kumi katika vita kule Bezeki.


Basi, Daudi alibaki katika makimbilio ndani ya jangwa, katika inchi ya milima ya mbuga za Zifu. Saulo alimutafuta kila siku, lakini Mungu hakumutia Daudi katika mikono yake.


Saulo alipokuwa anasafiri, alifika kwenye pango moja lililokuwa karibu na zizi la kondoo, akaingia mule ndani ya pango kwa kujisaidia. Daudi na watu wake walikuwa wakiikaa ndani kabisa ya pango lile.


Watu wa Daudi wakamwambia: “Ile siku Yawe aliyokuambia kwamba atakuja kumutia adui yako katika mikono yako nawe umutendee utakavyoona inafaa, leo imefika.” Halafu Daudi alimwendea Saulo polepole kutoka nyuma, akakata pindo la nguo yake.


Yawe anamulinda kila mutu kwa haki yake na uaminifu wake. Leo Yawe alikutia katika mikono yangu, lakini mimi sikunyoosha mukono wangu juu ya yule ambaye ni muchaguliwa wa Yawe.


Kwa hiyo usiku, Daudi na Abisai wakaingia kwenye kambi ya Saulo, wakamukuta Saulo amelala katikati ya kambi hiyo, na mukuki wake umechomekwa katika udongo karibu na kichwa chake. Abeneri pamoja na waaskari walikuwa wamelala na kumuzunguka Saulo.


Lakini Daudi akamwambia Abisai: “Usimwangamize; maana nani anaweza kunyoosha mukono wake juu ya mutu ambaye ni muchaguliwa wa Yawe, naye asiazibiwe?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ