Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 26:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Yawe anamulinda kila mutu kwa haki yake na uaminifu wake. Leo Yawe alikutia katika mikono yangu, lakini mimi sikunyoosha mukono wangu juu ya yule ambaye ni muchaguliwa wa Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 26:23
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe alinitendea kwa kadiri ya haki yangu; alinilipa kwa vile mikono yangu haina kosa.


Yawe amenilipa kwa kadiri ya haki yangu, kwa kadiri ya usafi wangu mbele yake.


tafazali wewe usikilize kutokea kule mbinguni, utende na kuwahukumu watumishi wako. Anayekuwa na kosa umwazibu kwa kadiri ya makosa yake; asiyekuwa na kosa umwachilie na kumupatia haki kwa kadiri ya haki yake.


Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya haya yote na usiyasahau matendo yangu mema niliyofanya kwa ajili ya nyumba yako na kwa ajili ya kazi yako.


Mungu atamulipa mutu kadiri ya matendo yake, atamulipiza kulingana na mwenendo wake.


Mungu amesema mara na mara, nami nimesikia tena na tena kwamba uwezo ni wa Mungu.


Sasa, leo umejionea kwa macho yako mwenyewe. Ulipokuwa ndani ya pango Yawe alikutia katika mikono yangu. Wamoja kati ya watu wangu waliniambia nikuue, lakini nilikuhurumia. Nikasema sitanyoosha mukono wangu juu ya bwana wangu maana yeye ni muchaguliwa wa Yawe.


Angalia, baba yangu, angalia pindo hili la nguo yako katika mikono yangu. Kwa kulikata pindo la nguo yako bila kukuua, unaweza sasa kujua kwa hakika kwamba mimi si mwovu wala mwasi. Mimi sijatenda zambi juu yako ingawa wewe unaniwinda uniue.


Kisha akamwambia Daudi: “Wewe una haki kuliko mimi; umenilipa mazuri, wakati mimi nimekulipa mabaya.


Leo, umeonyesha jinsi unavyokuwa muzuri kwangu. Haukuniua ijapokuwa Yawe alinitia katika mikono yako.


Lakini Yawe anakataza nisinyooshe mukono wangu juu ya mutu ambaye ni muchaguliwa wa Yawe. Lakini twaa mukuki wake unaokuwa karibu na kichwa chake pamoja na mufuko wake wenye maji, halafu tujiendee zetu.”


Daudi akajibu: “Ee mufalme, mukuki wako uko hapa, utume kijana wako mumoja akuje aukamate.


Lakini Daudi akamwambia Abisai: “Usimwangamize; maana nani anaweza kunyoosha mukono wake juu ya mutu ambaye ni muchaguliwa wa Yawe, naye asiazibiwe?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ