Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 26:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Halafu Saulo akajibu: “Mimi nimefanya makosa. Rudi mwana wangu Daudi. Sitakuzuru tena kwa sababu leo maisha yangu yalikuwa ya bei kali mbele yako. Mimi nimekuwa mupumbafu na nimekosa vibaya sana.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 26:21
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa mara ingine tena, mufalme akatuma kiongozi mwingine na watu wake makumi tano. Kiongozi wa tatu akapanda kwenye mulima, akapiga magoti mbele ya Elia na kumusihi akisema: “Ewe mutu wa Mungu, ninakusihi uyahesabu maisha yangu na maisha ya hawa watumishi wako makumi tano yakuwe ya bei kali mbele yako.


Viongozi wawili waliotangulia na watu wao, wameteketezwa na moto ulioshuka toka mbinguni; lakini sasa ninakuomba uhurumie maisha yangu.”


Kifo cha waaminifu wa Yawe si jambo dogo mbele yake.


Lakini mwanadamu hawezi hata kidogo kujikomboa mwenyewe; hawezi kumulipa Mungu bei ya maisha yake,


Atawatoa katika mateso na ukali, maana maisha yao ni ya bei kubwa kwake.


Basi, mufalme wa Misri akaagiza Musa na Haruni waitwe, akawaambia: “Mara hii nimetenda zambi. Yawe ana haki na mimi na watu wangu tumekosa.


Balamu akamwambia malaika wa Yawe: Nimetenda zambi maana sikujua kwamba umesimama katika njia kwa kunizuia. Sasa, kama haikupendezi niendelee na safari hii, basi nitarudi kwangu.


Akawaambia: “Nimekosa kwa kumutoa mutu huyu asiyekuwa na kosa auawe.” Lakini wao wakamujibu: “Jambo hilo halituelekei. Ni kazi yako wewe mwenyewe!”


Samweli akamujibu Saulo: “Umefanya kipumbafu. Haukutii mambo Yawe, Mungu wako, aliyokuamuru. Kama ungetii, Yawe angeudumisha milele ufalme wako juu ya Israeli.


Saulo akamwambia Samweli: “Nimetenda zambi. Nimeasi amri ya Yawe na amri yako, kwa sababu niliwaogopa watu, nikawatii wao.


Saulo akajibu: “Nimefanya zambi. Hata hivyo, uniheshimishe sasa mbele ya wazee wa watu wangu na Waisraeli. Uniruhusu nirudi pamoja nawe kusudi nimwabudu Yawe, Mungu wako.”


Waaskari wa Wafilistini walikwenda kupigana na Waisraeli, lakini kila mara walipopigana vita, Daudi alipata ushindi kuliko watumishi wa Saulo. Hivyo jina la Daudi likazidi kusifiwa sana.


Daudi alipomaliza kusema, Saulo akasema: “Hiyo ni sauti yako mwana wangu Daudi?” Saulo akalia kwa sauti.


Daudi akajibu: “Ee mufalme, mukuki wako uko hapa, utume kijana wako mumoja akuje aukamate.


Angalia kama vile leo maisha yako yalivyokuwa na bei kali mbele yangu, ndivyo maisha yangu yapate kuwa na bei kali mbele ya Yawe; naye aniokoe kutoka taabu zote.”


Saulo aliposikia kwamba Daudi amekimbilia Gati, hakumufuata tena.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ