Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 26:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kama vile Yawe anavyoishi, Yawe mwenyewe atamwua, au siku yake ya kufa itamufikia au atakuja kwenda katika vita na kuangamizwa kule.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 26:10
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati wa kufa kwake ulipokaribia, Yakobo akamwita mwana wake Yosefu, akamwambia: “Sasa, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, weka mukono wako chini ya mapaja yangu, uniahidi kwamba utanitendea kwa wema na uaminifu. Usinizike huku Misri,


Mutu akikufa anaweza kuishi tena? Siku zangu zote za kazi ningekungoja mpaka wakati wa kufunguliwa ufike.


Siku za kuishi za mwanadamu zimepimwa. Ee Mungu, umepanga hesabu ya miezi yake; hawezi kupita mupaka uliomwekea.


Mwanadamu ana magumu katika dunia, na siku zake ni kama siku za mutumishi wa mushahara!


Bado kidogo, mwovu atatoweka; utamutafuta pale alipokuwa, wala hautamwona.


Lakini Yawe anamuchekelea mwovu, kwa maana anajua mwisho wake ni karibu.


Atawarudishia uovu wao wenyewe, atawateketeza kwa sababu ya ubaya wao. Yawe, Mungu wetu, atawateketeza kabisa!


wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna kilichopandwa,


Basi, Mungu hatawapatia haki wale wachaguliwa wake wanaomulilia usiku na muchana? Au atakawia kuwasaidia?


Wandugu wapendwa, musilipize kisasi ninyi kwa ninyi, lakini mumwachie Mungu wakati wa kutenda kufuatana na kasirani, maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ni kazi yangu kulipiza kisasi. Ni mimi nitakayelipiza.”


Yawe akamwambia Musa: “Siku yako ya kuaga dunia imekaribia. Umwite Yoshua, mukuje pamoja katika hema la mukutano kusudi nimupe maagizo.” Basi, Musa na Yoshua wakaenda katika hema la mukutano,


Ni kazi yangu kulipiza kisasi, mimi nitalipiza, wakati miguu yao itakapoteleza; maana siku yao ya hasara imefika mwisho wao uko karibu sana.


Kwa maana tunamujua yule aliyesema: “Ni kazi yangu kulipiza kisasi. Ni mimi nitakayelipiza.” Naye alisema tena: “Bwana atawahukumu watu wake.”


Kila mutu anapaswa kufa mara moja tu, na nyuma ya kufa, anahukumiwa na Mungu.


Kwa sababu hiyo, kwa muda wa siku moja tu utapatwa na mapigo ya mauti, huzuni na njaa. Na zaidi ya hiyo utateketezwa kwa moto, kwa maana Bwana wetu, Mungu anayeuhukumu, ni mwenye uwezo.”


Angalia, baba yangu, angalia pindo hili la nguo yako katika mikono yangu. Kwa kulikata pindo la nguo yako bila kukuua, unaweza sasa kujua kwa hakika kwamba mimi si mwovu wala mwasi. Mimi sijatenda zambi juu yako ingawa wewe unaniwinda uniue.


Sasa wewe mufalme wa Israeli angalia mutu unayetaka kumwua! Unamufuatilia nani? Unafuatilia imbwa yenye kufa! Unakifuatilia kiroboto!


Sasa bwana wangu, kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, unaona kwamba Yawe amekuzuia kulipiza kisasi kwa kumwanga damu na hivyo upate kuwa na kosa. Uwaache waadui zako na wale wote wanaokutakia mabaya wakuwe wapumbafu kama Nabali.


Kisha siku kumi, Yawe alimupiga Nabali akakufa.


Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, alisema: “Atukuzwe Yawe ambaye amemulipiza kisasi Nabali kwa kunitukana, naye Yawe ameniepusha mimi mutumishi wake kutenda maovu. Yawe amemwazibu Nabali kwa uovu wake.” Kisha Daudi alituma watu kwa kumuchumbilia Abigaili akuwe muke wake.


Halafu Saulo akamwambia mutu aliyemubebea silaha: “Chomoa upanga wako unichome nikufe, kusudi watu hawa wapagani wasikuje kunichoma upanga na kunichekelea.” Lakini yule aliyemubebea silaha hakusubutu kwa sababu aliogopa sana. Kwa hiyo, Saulo alitwaa upanga wake mwenyewe, na kuuangukia.


Hivi ndivyo Saulo alivyokufa na wana wake watatu, vilevile na mutu aliyemubebea silaha pamoja na watu wake wote katika siku ileile moja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ