Wale wanafunzi wa manabii kutoka Yeriko walipomwona, walisema: “Roho wa Elia yuko kwa Elisha.” Basi, wakaenda kumupokea, wakainama mbele yake kwa heshima.
Mufalme Asa alikuwa na jeshi la waaskari elfu mia tatu kutoka Yuda, wenye ngao na mikuki, na wengine elfu mia mbili na makumi nane kutoka katika kabila la Benjamina, wenye ngao na pinde. Wote walikuwa watu mashujaa sana.
Ukiwauliza, watakuambia. Sasa ninakuomba vijana wangu hawa wapate kukubaliwa mbele yako, maana tumefika wakati wa sikukuu. Tafazali uwapatie kitu chochote unachokuwa nacho watumishi wako hawa nami mwana wako Daudi.’ ”