Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 25:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Nimesikia kwamba unawakata kondoo wako manyoya. Ninataka ujue kwamba wachungaji wako walikuwa pamoja nasi, nasi hatukuwazuru. Tena muda wote walipokuwa pamoja nasi katika muji wa Karmeli, hawakukosa kitu chochote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 25:7
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya miaka miwili mizima, Abusaloma alikuwa na shuguli ya kuwakata kondoo wake manyoya katika muji wa Bali-Hazori, karibu na Efuraimu. Akawaalika wana wote wa mufalme.


Abusaloma alimwendea mufalme Daudi, akamwambia: “Angalia, mimi mutumishi wako ninawakata kondoo manyoya. Ninakuomba wewe mufalme pamoja na watumishi wako, muende pamoja nami, mutumishi wako.”


Nao waaskari wakamwuliza: “Na sisi, tufanye nini?” Naye akawajibu: “Musifanye ukorofi kwa mutu yeyote wala kumusingizia mutu, lakini mutoshelewe na mishahara yenu.”


kusudi mupate kuwa bila kosa na kuwa na maisha safi. Hivi mutakuwa watoto wakamilifu wa Mungu wasiokuwa na kilema kati ya watu waovu na wapotovu wa dunia hii. Munapaswa kuangaza kati ya watu hawa kama vile nyota zinavyoangaza katika mbingu,


Kwa kumaliza, wandugu zangu, muweke mafikiri yenu juu ya mambo yote yanayokuwa ya kweli, ya heshima, ya haki, safi, ya kupendeza, nayo mambo yote yanayostahili sifa na ya utu wema.


Watu wote waliogandamizwa au waliokuwa na madeni au wale wenye huzuni walijiunga na Daudi. Jumla yao ilikuwa watu yapata mia ine, naye akakuwa kiongozi wao.


Daudi alikuwa akifikiri: “Mimi nimekuwa nikilinda mali yote ya Nabali katika jangwa bila faida yoyote na hakuna kitu chake chochote kilichopotea, naye amenilipa mabaya kwa mazuri niliyomutendea.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ