Yule musimamizi akawajibu: “Musikuwe na wasiwasi, wala musiogope. Bila shaka Mungu wenu, Mungu wa baba yenu, ndiye aliyewarudishia feza katika mifuko yenu. Mimi nilipokea feza yenu.” Kisha akawaletea Simeoni, ndugu yao.
Halafu Ahimasi akamwambia mufalme kwa sauti kubwa: “Mambo yote ni sawa.” Akainama mbele ya mufalme, kwa heshima na kusema: “Yawe atukuzwe, Mungu wako, ambaye amekukomboa kutoka watu walioinua mikono yao juu yako, bwana wangu mufalme.”
Daudi akatoka inje kwa kuwapokea, akawaambia: “Ikiwa mumekuja kwangu kama warafiki kwa kunisaidia basi ninawapokea kwa moyo wote, lakini kama mumekuja kwa kunitoa kwa waadui zangu, ingawa sijatenda ovu lolote, Mungu wa babu zetu awaone na kuwaazibu ninyi.”