Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.
Hapo Ruta akamwinamia Boazi uso mpaka chini kwa unyenyekevu, akamwambia: “Nimepata namna gani kukubaliwa mbele yako? Mbona unanishugulikia ijapokuwa mimi ni mugeni tu?”
Ruta akamujibu: “Bwana, wewe umenifanyia wema mukubwa sana. Ingawa mimi si kama mumoja wa watumishi wako, nimetosheka kwa sababu umenifariji sana na kuongea nami kwa upendo.”