Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 25:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, alisema: “Atukuzwe Yawe ambaye amemulipiza kisasi Nabali kwa kunitukana, naye Yawe ameniepusha mimi mutumishi wake kutenda maovu. Yawe amemwazibu Nabali kwa uovu wake.” Kisha Daudi alituma watu kwa kumuchumbilia Abigaili akuwe muke wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 25:39
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi akasema: “Ubebe wewe mwenyewe lazima ya kifo chako, maana umejishuhudia wewe mwenyewe kwa kinywa chako mwenyewe ukisema: ‘Nimemwua muchaguliwa wa Yawe.’ ”


Mufalme aliendelea kumwambia Simei: “Unayajua wazi maovu uliyomutendea baba yangu Daudi. Sasa, kwa sababu ya hayo, Yawe atakuazibu.


Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.


Lakini Esteri alipomwendea mufalme, naye mufalme akatoa amri kwa waandishi kwamba lile shauri baya ambalo Hamani alikuwa amefanya juu ya Wayuda, limurudilie yeye mwenyewe; na ya kuwa yeye na wana wake wauawe kwa kutundikwa kwenye muti.


Anachimba shimo, na kulirefusha, kisha anatumbukia humo yeye mwenyewe.


Umeitetea haki yangu katika maneno yangu; umeikaa katika kiti chako cha kifalme, wewe mwamuzi wa haki.


Anayemupata muke amepata kizuri; ni zawadi kutoka kwa Yawe.


Nyumba na mali ni urizi mutu anaopata kwa babu zake, lakini muke mwenye akili anatoka kwa Yawe.


Maana Yawe atawatetea; atagandamiza maisha ya wale wanaowagandamiza.


Muke mwema atapatikana wapi? Bei yake ni kali kuliko ushanga!


Mapendezi ni udanganyifu na uzuri wa uso haukawii, lakini mwanamuke anayemwogopa Yawe atasifiwa.


Tuna dada mudogo, ambaye bado hajaota maziba. Basi, tutamufanyia dada yetu nini siku atakapochumbiwa?


Kwa vile nimemukosea Yawe, nitavumilia kasirani yake, mpaka atakapotetea maneno yangu na kunijalia haki yangu. Atanileta inje kwenye mwangaza, nami nitaona akisimamisha haki.


Nasi tunaomba Mungu kusudi musifanye jambo lolote baya, nasi hatutaki kuonyesha kwamba tumeshinda. Lakini tunataka mutende mema hata ikionekana kuwa sisi tunashindwa.


Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa, alinde uzima wenu wote ndiyo roho, moyo na mwili wenu, kusudi visikutiwe na kosa wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakaporudia.


Bwana ataniokoa toka katika mambo yote mabaya na kunipeleka salama katika Ufalme wake wa mbinguni. Bwana atukuzwe milele na milele. Amina.


Viongozi walijitokeza kuongoza Israeli, watu walijitolea kwa mapenzi yao. Mumushukuru Yawe!


Sasa wewe mufalme wa Israeli angalia mutu unayetaka kumwua! Unamufuatilia nani? Unafuatilia imbwa yenye kufa! Unakifuatilia kiroboto!


Sasa bwana wangu, kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, unaona kwamba Yawe amekuzuia kulipiza kisasi kwa kumwanga damu na hivyo upate kuwa na kosa. Uwaache waadui zako na wale wote wanaokutakia mabaya wakuwe wapumbafu kama Nabali.


Daudi akamwambia Abigaili: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli, aliyekutuma leo kukutana nami.


Kwa hakika, kama Yawe, Mungu wa Israeli, anavyoishi, amenizuia kukuzuru. Usingefanya haraka kuja kukutana nami, kwa hakika, kesho asubui hakuna mwanaume yeyote wa Nabali ambaye angebaki.”


Watumishi wa Daudi walipofika kwa Abigaili kule Karmeli, wakamwambia: “Daudi ametutuma kukutwaa kusudi ukuwe muke wake.”


Kama vile Yawe anavyoishi, Yawe mwenyewe atamwua, au siku yake ya kufa itamufikia au atakuja kwenda katika vita na kuangamizwa kule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ