Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 25:38 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

38 Kisha siku kumi, Yawe alimupiga Nabali akakufa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 25:38
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Uza. Mungu akamwua palepale. Uza akakufa palepale pembeni ya Sanduku la Mungu.


Yawe akamwazibu Azaria, akakuwa na ukoma mpaka alipokufa. Alikaa katika nyumba ya pekee na shuguli zake zote za utawala ziliendeshwa na mwana wake Yotamu.


Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


Halafu mufalme hakuwajali watu kwa sababu jambo hili lilisababishwa na Mungu kusudi Yawe atimize neno lake alilomwambia Yeroboamu, mwana wa Nebati kwa njia ya Ahiya wa Shilo.


Yeroboamu hakuweza kupata nguvu tena wakati wa Abiya. Kwa mwisho Yawe akamupiga, naye akakufa.


Ukiwageuzia mugongo, wanaogopa; ukiondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi ndani ya mavumbi walimotoka.


Wanaangamizwa kwa rafla, wateketezwe kabisa kwa vitisho.


Katikati ya usiku, Yawe akawaua wazaliwa wa kwanza wote wa Misri. Wote walikufa, tangu muzaliwa wa kwanza wa mufalme wa Misri, murizi wa ufalme, mpaka muzaliwa wa kwanza wa mufungwa katika kifungo. Hata wazaliwa wa kwanza wa nyama nao walikufa.


Na pale pale malaika wa Bwana akamwazibu Herode kwa ugonjwa kwa sababu alijitukuza kwa pahali pa Mungu. Herode akakuliwa na michango ya tumbo na kisha akakufa.


Umutukuze Yawe aliyekupa hekima kwa kunizuia kuwa na kosa la umwangaji wa damu na kujilipiza kisasi mimi mwenyewe.


Asubui, Abigaili alipoona kwamba divai imemutoka mume wake, alimwelezea mambo yote, na palepale Nabali akapooza, akakuwa kama jiwe.


Kama vile Yawe anavyoishi, Yawe mwenyewe atamwua, au siku yake ya kufa itamufikia au atakuja kwenda katika vita na kuangamizwa kule.


Lakini muangalie. Ikiwa gari hilo linakwenda moja kwa moja kuelekea inchi yake, ni kusema kwenye muji wa Beti-Semesi, basi, pale tutajua kwamba aliyetuletea pigo hili ni Mungu wa Israeli. Lakini kama haliendi kule, basi, tutajua kwamba sio mukono wake uliotupiga, lakini hasara hii imetupata kwa bahati mbaya.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ