Lakini mwizi akishikwa wakati jua limechomoza na kuuawa, aliyemwua atakuwa na kosa. Mwizi anapaswa kulipa. Ikiwa hana kitu cha kulipa, basi, yeye mwenyewe atauzishwa kwa kulipa kile alichoiba.
Sasa bwana wangu, kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, unaona kwamba Yawe amekuzuia kulipiza kisasi kwa kumwanga damu na hivyo upate kuwa na kosa. Uwaache waadui zako na wale wote wanaokutakia mabaya wakuwe wapumbafu kama Nabali.
wewe bwana wangu, hautakuwa na sababu ya kujuta wala kuhukumiwa na zamiri kutokana na kumwanga damu bila sababu kwa kujilipiza kisasi. Lakini, Yawe atakapokuwa amekutendea vizuri, ninakuomba, bwana wangu, unikumbuke mimi mujakazi wako.”