Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 25:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Ninakuomba unisamehe mimi mujakazi wako. Yawe atakupa jamaa imara kwa sababu, wewe bwana wangu, unapigana vita ya Yawe. Wakati wote wa maisha yako usipatikane na ubaya wowote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 25:28
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zamani, Saulo alipokuwa mufalme wetu wewe ndiwe uliyewaongoza Waisraeli katika vita, na Yawe alikuambia: ‘Utakuwa muchungaji wa watu wangu Waisraeli; utakuwa mukubwa juu ya inchi ya Israeli.’ ”


wakati nilipowachagua waamuzi juu ya watu wangu Waisraeli. Nami nitakulinda kutokana na waadui zako wote. Zaidi ya hayo, mimi Yawe ninakutangazia kwamba nitakujengea nyumba.


Ukoo wako na ufalme wako vitadumu imara siku zote. Kiti chako cha kifalme kitakuwa imara milele.”


Maana wewe, ee Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, umenifunulia mimi mutumishi wako, ukisema: ‘Nitakujengea nyumba’; ndiyo maana nina uhodari wa kutoa ombi hili mbele yako.


Abiyamu alitenda zambi zilezile baba yake alizotenda, wala hakukuwa na moyo mwaminifu kwa Yawe, Mungu wake, kama babu yake Daudi alivyokuwa.


Yawe alifanya hivyo kwa sababu Daudi alitenda mema mbele yake na hakuenda pembeni ya maagizo ya Yawe siku za maisha yake yote, isipokuwa tu lile jambo la Uria Muhiti.


basi, mimi nitakiimarisha kiti chako cha kifalme juu ya Israeli milele, kama nilivyomwahidi baba yako Daudi, nikisema: Hautakosa mutu wa kuikaa juu ya kiti cha kifalme cha Israeli.


wakati nilipowachagua waamuzi juu ya watu wangu Waisraeli. Mimi nitawashinda waadui zako wote. Zaidi ya yote, mimi Yawe ninakutangazia kwamba nitakupa wazao.


Maana, ee Mungu wangu, nimepata bidii ya kukuomba kwa sababu umenifunulia ukisema kwamba utanipa wazao.


Yahazieli akasema: “Musikilize ninyi watu wa Yuda na wakajii wa Yerusalema na mufalme Yosafati, Yawe anawaambia hivi: musiogope wala musihangaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Vita hivi si vyenu, lakini ni vya Mungu.


Kama si vile, watakuja kunirarua kama simba, kunipasua vipandevipande wala hakuna wa kuniokoa.


Nitamwonyesha wema wangu kwa milele, na agano langu kwake litadumu siku zote.


Yawe hajaona ubaya kwa watu wa Yakobo, wala uovu kwa hao watu wa Israeli. Yawe Mungu wao yuko pamoja nao, Yeye anasifiwa kwa vigelegele kati yao, yeye anapokea sifa zao za kifalme.


Vilevile, mwangaza wenu unapaswa kuangaza mbele ya watu, kusudi waone matendo yenu mazuri, nao wamutukuze Baba yenu anayekuwa mbinguni.


Sisi tunahukumiwa kwa haki, kwa maana tunaazibiwa kufuatana na matendo yetu mabaya. Lakini mutu huyu hakufanya ubaya wowote.”


Mukubwa wa waaskari alipoona mambo yale yaliyotokea, akamusifu Mungu, akisema: “Hakika mutu huyu alikuwa mwenye haki!”


Halafu Samweli akamwambia Saulo: “Tangu leo Yawe ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako na atamupa mutu mwingine kati ya wajirani zako anayekuwa bora kuliko wewe.


Watu wote waliokusanyika hapa leo, watajua kwamba Yawe hahitaji mikuki kwa kuwaokoa watu. Hii ni vita ya Yawe, naye atawatia ninyi wote katika mikono yetu.”


Saulo akamwambia Daudi: “Huyu ni Merabu, binti yangu mukubwa, nitamutoa kwako kusudi umwoe kwa masharti mawili: Ukuwe askari wangu shujaa na mutiifu, upigane vita ya Yawe.” Saulo alizani kwa njia hiyo Wafilistini watamwua Daudi, kusudi kitendo hicho asikifanye yeye mwenyewe.


Kisha, nitajiinulia kuhani mwingine mwaminifu atakayefanya kulingana na yale yanayokuwa ndani ya moyo na akili yangu. Nitamujengea ukoo imara, naye atatumika siku zote mbele ya mufalme wangu muchaguliwa.


Ahimeleki akamujibu: “Kati ya watumishi wako, Daudi ndiye mukubwa wa kuaminika kuliko wote. Yeye ni mukwe wako wewe mufalme mwenyewe, mukubwa wa waaskari wako walinzi na anaheshimiwa kuliko wote katika nyumba yako.


Sasa, leo umejionea kwa macho yako mwenyewe. Ulipokuwa ndani ya pango Yawe alikutia katika mikono yangu. Wamoja kati ya watu wangu waliniambia nikuue, lakini nilikuhurumia. Nikasema sitanyoosha mukono wangu juu ya bwana wangu maana yeye ni muchaguliwa wa Yawe.


Daudi alipomaliza kusema, Saulo akasema: “Hiyo ni sauti yako mwana wangu Daudi?” Saulo akalia kwa sauti.


Sasa nimejua kwamba hakika utakuwa mufalme wa Israeli, na ufalme wa Israeli utaimarishwa chini yako.


Saulo alipokuwa anasafiri, alifika kwenye pango moja lililokuwa karibu na zizi la kondoo, akaingia mule ndani ya pango kwa kujisaidia. Daudi na watu wake walikuwa wakiikaa ndani kabisa ya pango lile.


Alijitupa kwenye miguu ya Daudi na kumwambia: “Bwana wangu, kosa lote likuwe juu yangu tu. Ninakuomba niongee nawe mimi mujakazi wako. Ninakuomba usikilize maneno ya mujakazi wako.


Wakubwa wa waaskari wa Wafilistini waliuliza: “Waebrania hawa wanafanya nini hapa?” Akisi akawajibu wale wakubwa wa Wafilistini: “Huyu ni Daudi, mutumishi wa Saulo mufalme wa Israeli; naye amekuwa nami kwa miaka fulani. Na tangu alipokimbilia kwangu, sijamupata na kosa lolote.”


Daudi aliporudia Ziklagi, aliwapelekea warafiki zake ambao ni wazee wa Yuda sehemu ya vitu akisema: “Ninawaletea zawadi kutoka katika vitu vya waadui wa Yawe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ