Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 25:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Sasa bwana wangu, kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, unaona kwamba Yawe amekuzuia kulipiza kisasi kwa kumwanga damu na hivyo upate kuwa na kosa. Uwaache waadui zako na wale wote wanaokutakia mabaya wakuwe wapumbafu kama Nabali.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 25:26
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Mungu akamwambia katika hiyo ndoto: “Sawa. Ninajua kwamba umefanya hivyo kwa moyo safi. Mimi ndiye niliyekuzuia kutenda zambi mbele yangu. Ndiyo maana sikukuruhusu umuguse huyo mwanamuke.


Mufalme akamwuliza: “Kijana Abusaloma ni muzima?” Mwetiopia akasema: “Waadui zako, bwana wangu mufalme, pamoja na wote wanaokushambulia wakikutakia mabaya, wakuwe kama huyo kijana Abusaloma.”


Walipokuwa katika njia, Elia akamwambia Elisha: “Tafazali ubakie hapa. Yawe amenituma niende Beteli.” Lakini Elisha akamwambia: “Kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, sitakuacha.” Basi, wakaenda pamoja mpaka Beteli.


Vilipojaa vyote, akamwambia mwana wake mumoja: “Uniletee chombo kingine.” Mwana wake akamujibu: “Vyote vimejaa!” Hapo mafuta yakakoma kutiririka.


Kwa mukono wako mwenyewe uliyafukuza mataifa, na mahali pao ukawaikalisha watu wako; uliyaazibu mataifa, na kuwafanikisha watu wako.


Hamutendei mume wake mabaya hata kidogo, lakini anamutendea mazuri maisha yake yote.


Kwa sababu jambo hilo litakalowapata, watu wote waliohamishiwa Babeli kutoka Yuda, watatumia mufano huu kwa kutoa laana: Yawe akufanye kama Zedekia na Ahabu, ambao mufalme wa Babeli aliwachoma katika moto.


basi, ni wewe, ee mufalme, ambaye umekuwa mukubwa na mwenye nguvu. Ukubwa wako umefika mpaka mbinguni, na ufalme wako umeenea mpaka miisho ya dunia.


Kwa maana tunamujua yule aliyesema: “Ni kazi yangu kulipiza kisasi. Ni mimi nitakayelipiza.” Naye alisema tena: “Bwana atawahukumu watu wake.”


Hana akamwambia: “Ee bwana wangu, kama vile unavyoishi, bwana wangu, mimi ni yule mwanamuke aliyekuwa anasimama mbele yako akimwomba Yawe.


Anayalinda maisha ya waaminifu wake, lakini anaangamiza maisha ya waovu katika giza. Maana, mwanadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.


ninaomba jina langu lisikatiliwe kabisa kutoka katika jamaa yako. Yawe awalipize kisasi waadui zako.”


Daudi akaapa vilevile: “Hakika baba yako anajua vizuri kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako. Anafikiri kukuficha juu ya jambo hili kusudi usihuzunike atakapolitenda. Lakini kweli, kama Yawe anavyoishi na kama wewe mwenyewe unavyoishi, kati yangu na lufu kuna hatua moja tu!”


Kutoka kule, Daudi alikwenda mpaka Misipa katika inchi ya Moabu. Akamwambia mufalme wa Moabu: “Tafazali, baba yangu na mama yangu wakae hapa kwako mpaka nijue Mungu atanifanyia nini.”


Usimwangalie Nabali ambaye ni mutu mubaya. Maana jina lake la Nabali linamustahili. Yeye anaitwa Nabali; na kweli yeye ni mutu mupumbafu. Bwana wangu, wale vijana wako ulipowatuma, mimi mujakazi wako sikuwaona.


Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, alisema: “Atukuzwe Yawe ambaye amemulipiza kisasi Nabali kwa kunitukana, naye Yawe ameniepusha mimi mutumishi wake kutenda maovu. Yawe amemwazibu Nabali kwa uovu wake.” Kisha Daudi alituma watu kwa kumuchumbilia Abigaili akuwe muke wake.


Kama vile Yawe anavyoishi, Yawe mwenyewe atamwua, au siku yake ya kufa itamufikia au atakuja kwenda katika vita na kuangamizwa kule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ