Zaidi ya yote, mutamwambia: ‘Mutumishi wako Yakobo yuko nyuma, anafuata.’ ” Yakobo alifanya hivyo akifikiri: “Pengine nitamutuliza kwa zawadi hizi ninazomutangulizia na kisha nitaweza kuonana naye macho kwa macho; labda atanipokea.”
Siku moja, Yonatani mwana wa mufalme Saulo alimwambia kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende ngambo kwenye kambi ya Wafilistini.” Lakini Yonatani hakumwambia baba yake.
Alipokuwa anateremuka, akipanda juu ya punda wake, na kukingwa na mulima upande mumoja, akakutana kwa rafla na Daudi na watu wake wakiwa wanaelekea upande anakotoka.
Abigaili aliporudi kwake, alimukuta Nabali akifanya karamu kubwa katika nyumba yake kama ya kifalme. Nabali alikuwa akifurahi sana ndani ya moyo maana alikuwa amelewa sana. Kwa hiyo hakumwambia neno lolote mpaka asubui.