Gideoni akarudi kwa watu wa Sukoti, akawaambia: “Si mutakumbuka mulivyonitukana muliposema: ‘Kwa nini tuwape mikate watu wako waliochoka sana nanyi hamujamushinda Sadaka na Kivuli?’ Haya basi, Sadaka na Kivuli ndio hawa.”
Mutu yule aliitwa Nabali na muke wake aliitwa Abigaili. Abigaili alikuwa mwanamuke mwenye akili na sura nzuri. Lakini Nabali alikuwa mutu wa chuki na mutenda maovu; tena alikuwa wa ukoo wa Kalebu.
Nimesikia kwamba unawakata kondoo wako manyoya. Ninataka ujue kwamba wachungaji wako walikuwa pamoja nasi, nasi hatukuwazuru. Tena muda wote walipokuwa pamoja nasi katika muji wa Karmeli, hawakukosa kitu chochote.