Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 25:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Sasa, Samweli akakufa. Nao Waisraeli wote wakakusanyika kwa kumwomboleza. Wakamuzika kwenye nyumba yake kule Rama. Kisha Daudi akaenda zake kwenye jangwa za Parani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 25:1
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

na Wahori kule kwenye mulima wa Seiri, wakawafukuza mpaka Eliparani, kwa mupaka wa jangwa.


Alikuwa akikaa katika jangwa za Parani, na mama yake akamwoea muke kutoka inchi ya Misri.


Alikufia kule Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya Kanana. Abrahamu akaomboleza na kumufanyia Sara muke wake kilio.


Wakanana wenyeji wa inchi hiyo, walipoona maombolezo yaliyofanyika kwenye uwanja wa kupepetea ngano wa Atadi, wakasema: “Maombolezo haya ya Wamisri, kweli ni makubwa!” Kwa hiyo, pahali pale pakaitwa Abeli-Misri, napo pako ngambo ya muto Yordani.


Basi, Benaya mwana wa Yehoyada akaenda katika hema, akamwua Yoabu ambaye alizikwa katika shamba lake, katika mbuga.


Manase akakufa na kuzikwa katika bustani ya nyumba yake mwenyewe, katika Bustani ya Uza. Naye mwana wake Amoni akatawala kwa pahali pake.


Manase alikufa na kuzikwa katika nyumba yake ya kifalme, naye Amoni, mwana wake, akatawala pahali pake.


Ole wangu maana ninaishi kama mugeni huko Meseki; ninaishi kama mugeni katika mahema ya Kedari.


Wafalme wote wa mataifa wamezikwa kwa heshima kila mumoja ndani ya kaburi lake.


Babu zenu, wako wapi? Na manabii, wanaishi milele?


nao Waisraeli wakaanza safari yao kutoka jangwa la Sinai. Wingu hilo likapanda na kisha likatua katika jangwa la Parani.


Nyuma ya hayo, watu wakafanya safari kutoka Haseroti, wakapiga kambi katika jangwa la Parani.


Wakawaendea Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja kule Kadesi, katika jangwa la Parani, wakatoa habari ya mambo waliyoona na kuwaonyesha matunda ya inchi.


Basi, kwa agizo la Yawe, Musa akatuma watu kutoka jangwa la Parani. Watu wote waliotumwa walikuwa viongozi wa makabila mbalimbali ya watu wa Israeli.


Waisraeli walipoona kwamba Haruni amekufa, wakafanya kilio cha siku makumi tatu.


Watu wenye kuogopa Mungu wakamuzika Stefano na kumufanyia kilio kikubwa.


Waisraeli wakaomboleza kifo chake kwa muda wa siku makumi tatu kwenye inchi ya bonde la Moabu. Kisha siku za kilio na maombolezo ya kifo chake zikaisha.


Kesho yake asubui, Elekana na jamaa yake waliamuka asubui mapema, na kisha kumwabudu Yawe, walirudi kwao Rama. Elekana akalala na muke wake Hana na Yawe akamukumbuka.


Wakati ule, Samweli alikuwa amekwisha kufa, na Waisraeli wote walikuwa wamekwisha kumwombolezea na kumuzika katika muji wake Rama. Saulo alikuwa amewafukuza kutoka katika inchi wenye kutabiri na wachawi.


Kisha, alikuwa akirudi Rama, maana kule ndiko kulikuwa kwake. Aliwaamulia Waisraeli haki zao kule, na kumujengea Yawe mazabahu kule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ