Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 24:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kwa maneno hayo, Daudi akawashawishi watu wake wasimuzuru Saulo; aliwakataza wasimushambulie. Kisha Saulo akasimama, akatoka ndani ya pango akaendelea na safari yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 24:8
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abramu akaanguka uso mpaka chini. Naye Mungu akamwambia:


Batiseba akainama uso mpaka chini, kwa heshima mbele ya mufalme, na kusema: “Bwana wangu mufalme Daudi aishi milele!”


Uwaheshimu baba yako na mama yako, kusudi uishi maisha marefu katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Mumupe kila mutu haki yake: mulipishaji wa kodi, mumulipe kodi; mulipishaji wa ushuru, mumulipe ushuru. Mumuheshimu anayestahili kuheshimiwa na mumutukuze anayestahili kutukuzwa.


Muwaheshimu watu wote. Muwapende wandugu zenu waamini. Mumwogope Mungu, mumuheshimu mufalme.


Yule kijana alipokwisha kuondoka, Daudi akasimama na kutoka pahali alipojificha karibu na lundo la mawe. Aliinama chini kwa heshima mara tatu mbele ya Yonatani. Wote wawili, Daudi na Yonatani, wakakumbatiana na kulia. Daudi alikuwa na uchungu zaidi kuliko Yonatani.


Akawaambia watu wake: “Yawe anizuie nisimutendee kitendo kama hiki bwana wangu ambaye ni muchaguliwa wa Yawe. Nisiunyooshe mukono wangu juu ya mutu ambaye Yawe amemupakaa mafuta.”


Kisha, Daudi naye akasimama, akatoka ndani ya pango na kumwita Saulo: “Bwana wangu mufalme!” Mufalme Saulo alipoangalia nyuma, Daudi aliinama mpaka chini, kwa kumuheshimu Saulo.


Saulo alitambua sauti ya Daudi, akamwuliza: “Hiyo ni sauti yako mwana wangu Daudi?” Daudi akamujibu: “Bwana wangu mufalme, ni sauti yangu.”


Saulo akamwambia yule mwanamuke: “Ni mufano wa nani?” Yule mwanamuke akamwambia: “Mwanaume muzee anapanda juu, naye anajifunika kanzu.” Halafu, Saulo akatambua kwamba yule ni Samweli. Saulo akainama uso mpaka chini, kwa heshima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ