Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 24:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Sasa wewe mufalme wa Israeli angalia mutu unayetaka kumwua! Unamufuatilia nani? Unafuatilia imbwa yenye kufa! Unakifuatilia kiroboto!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 24:15
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Yoasi akasahau mema yote aliyotendewa na Yoyada, baba ya Zakaria, akamwua mwana wake. Alipokuwa karibu kufa, alisema: “Yawe uangalie mambo haya na kuyalipiza.”


Unitetee na kunikomboa; unirudishie uzima kama ulivyoahidi.


Zaburi ya Daudi. Uwapinge, ee Yawe, hao wanaonipinga; uwashambulie hao wanaonishambulia.


Unipatie haki yangu, ee Mungu; uyatetee maneno yangu mbele ya watu wabaya; uniokoe na watu waongo na waovu.


Musikilize enyi watu wote; sikiliza ewe dunia na vyote vinavyokuwa ndani yako. Bwana wetu Yawe anakuja kuwashitaki, Bwana wetu anasema kutoka hekalu lake takatifu.


Kwa vile nimemukosea Yawe, nitavumilia kasirani yake, mpaka atakapotetea maneno yangu na kunijalia haki yangu. Atanileta inje kwenye mwangaza, nami nitaona akisimamisha haki.


Mimi sijakukosea kitu na ndiyo maana unafanya kosa unaponishambulia. Yawe ambaye ndiye Mwamuzi ataamua leo hii kati ya Waisraeli na watu wa Amoni.”


Goliati akamwuliza Daudi: “Sasa, hiyo fimbo ni ya nini? Unazani mimi ni imbwa hata unifikie kwa fimbo?” Mufilistini yule akamulaani Daudi kwa miungu yake.


Angalia, baba yangu, angalia pindo hili la nguo yako katika mikono yangu. Kwa kulikata pindo la nguo yako bila kukuua, unaweza sasa kujua kwa hakika kwamba mimi si mwovu wala mwasi. Mimi sijatenda zambi juu yako ingawa wewe unaniwinda uniue.


Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, alisema: “Atukuzwe Yawe ambaye amemulipiza kisasi Nabali kwa kunitukana, naye Yawe ameniepusha mimi mutumishi wake kutenda maovu. Yawe amemwazibu Nabali kwa uovu wake.” Kisha Daudi alituma watu kwa kumuchumbilia Abigaili akuwe muke wake.


Usiniache nikufe katika inchi ya kigeni, mbali na Yawe. Kwa nini wewe mufalme wa Israeli umetoka kuyatafuta maisha yangu kama mutu anayewinda kwale juu ya milima?”


alituma wapelelezi, akafahamishwa kwamba ni kweli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ