1 Samweli 24:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200211 Sasa, leo umejionea kwa macho yako mwenyewe. Ulipokuwa ndani ya pango Yawe alikutia katika mikono yangu. Wamoja kati ya watu wangu waliniambia nikuue, lakini nilikuhurumia. Nikasema sitanyoosha mukono wangu juu ya bwana wangu maana yeye ni muchaguliwa wa Yawe. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
na kuwaambia kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ole kwenu ninyi wanawake munaoshona vitepe vyenye hirizi ambavyo kila mutu anavivaa kwenye maunganio ya mikono na kutengeneza vitambaa vyenye hirizi za kila kimo kwa ajili ya watu wa kila umri. Munapowinda maisha ya watu wangu munazani kwamba mutaokoa maisha yenu wenyewe?
Niko hapa, na kama nimefanya tendo lolote baya, basi, mutoe ushuhuda mbele ya Yawe na mbele ya mufalme wake muchaguliwa. Nimenyanganya ngombe dume au punda wa mutu yeyote? Nimemugandamiza mutu yeyote? Nimemutesa mutu yeyote? Nimepokea kituliro kwa mutu yeyote kusudi nifunge macho mbele ya matendo yake? Museme nami nitamurudishia kitu chochote kile.”