Mufalme Solomono akamwambia kuhani Abiatari: “Ondoka uende katika shamba lako, kule Anatoti. Unastahili kufa wewe. Lakini sasa, sitakuua kwa sababu ulilishugulikia Sanduku la Agano la Yawe ulipokuwa na baba yangu Daudi, ukateswa pamoja naye.”
Hivi ndivyo Waisraeli watakavyokuwa: watakaa kwa muda murefu bila mufalme au mukubwa; bila sadaka, wala nguzo za sanamu wala vyombo walivyotumia kwa kujua mapenzi ya Mungu.
Yeye atamutegemea kuhani Eleazari ambaye atamujulisha mapenzi yangu kwa kutumia jiwe la shauri. Kwa njia hii, Eleazari atamwongoza Yoshua na Waisraeli wote wanapotoka na wanapoingia.
Paulo na Barnaba walipotambua jambo lile wakakimbilia katika muji wa Listra na wa Derbe ndani ya wilaya ya Likaonia na katika sehemu za kandokando yake.
Kisha Daudi akaomba: “Ee Yawe, Mungu wa Israeli, kwa hakika mimi mutumishi wako, nimesikia kwamba Saulo anapanga kuja kuangamiza muji wa Keila kwa sababu yangu.