Nyuma ya mambo yale, Daudi alimwomba Yawe shauri, akasema: “Niende kwenye muji mumoja kati ya miji ya Yuda?” Yawe akamwambia: “Kwenda!” Daudi akamwuliza: “Niende katika muji gani?” Yawe akamujibu: “Kwenda kwenye muji wa Hebroni.”
Halafu Daudi akamwomba Mungu shauri: “Niende kuwashambulia Wafilistini? Utawatia katika mikono yangu?” Naye Yawe akamwambia: “Kwenda, nitawatia katika mikono yako.”
Gideoni akamwambia Mungu: “Tafazali, usinikasirikie. Ninakuomba niseme mara moja tena. Ninakuomba uniruhusu nitumie ngozi hii kwa kufanya jaribio lingine. Ninakuomba juu ya ngozi kukuwe kukavu, lakini kwenye udongo kukuwe umande.”
Yawe akamwambia Gideoni: “Kwa hao watu mia tatu waliokunywa kwa kulamba kama imbwa, nitawaokoa Waisraeli na kuwatia Wamidiani katika mikono yao. Lakini wale wengine wote warudie kwao.”
Lakini watu wa Daudi wakamwambia: “Kama tukiwa hapahapa katikati ya inchi ya Yuda tunaogopa, itakuwa namna gani basi tukienda Keila na kushambulia waaskari wa Wafilistini?”
Basi, Daudi akaenda Keila pamoja na watu wake, na kule akapigana na Wafilistini, akawaua Wafilistini wengi na kunyanganya ngombe wengi. Kwa hiyo Daudi aliwaokoa wakaaji wa Keila.