Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 23:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Daudi akamwomba tena Yawe shauri, naye Yawe akamwambia: “Simama uende Keila maana nitawatia Wafilistini katika mikono yako.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 23:4
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya mambo yale, Daudi alimwomba Yawe shauri, akasema: “Niende kwenye muji mumoja kati ya miji ya Yuda?” Yawe akamwambia: “Kwenda!” Daudi akamwuliza: “Niende katika muji gani?” Yawe akamujibu: “Kwenda kwenye muji wa Hebroni.”


Basi, Daudi alimwuliza Yawe shauri: “Niende kuwashambulia Wafilistini? Utawatia katika mikono yangu?” Naye Yawe akamwambia Daudi: “Kwenda, maana hakika nitawatia Wafilistini katika mikono yako.”


Lakini hili si jambo gumu kwa Yawe; yeye atawapa vilevile ushindi juu ya Moabu.


Halafu Daudi akamwomba Mungu shauri: “Niende kuwashambulia Wafilistini? Utawatia katika mikono yangu?” Naye Yawe akamwambia: “Kwenda, nitawatia katika mikono yako.”


Hapo, ninyi mutatokea kutoka kule mulikokuwa munavizia na kuuteka muji, maana Yawe, Mungu wenu, atautia muji huo katika mikono yenu.


Gideoni akamwambia Mungu: “Tafazali, usinikasirikie. Ninakuomba niseme mara moja tena. Ninakuomba uniruhusu nitumie ngozi hii kwa kufanya jaribio lingine. Ninakuomba juu ya ngozi kukuwe kukavu, lakini kwenye udongo kukuwe umande.”


Yawe akamwambia Gideoni: “Kwa hao watu mia tatu waliokunywa kwa kulamba kama imbwa, nitawaokoa Waisraeli na kuwatia Wamidiani katika mikono yao. Lakini wale wengine wote warudie kwao.”


Usiku ule, Yawe akamwambia Gideoni: “Kwenda uwashambulie katika kambi yao, maana nimewatia katika mikono yako.


Wakamwuliza Mungu tena: “Kuna mutu zaidi anayekuja?” Yawe akawajibu: “Anajificha kwenye mizigo.”


Basi, Daudi akamwomba Yawe shauri: “Niende kuwashambulia Wafilistini hawa?” Yawe akamujibu: “Ndiyo, kwenda kuwashambulia Wafilistini na kuuokoa muji wa Keila.”


Lakini watu wa Daudi wakamwambia: “Kama tukiwa hapahapa katikati ya inchi ya Yuda tunaogopa, itakuwa namna gani basi tukienda Keila na kushambulia waaskari wa Wafilistini?”


Basi, Daudi akaenda Keila pamoja na watu wake, na kule akapigana na Wafilistini, akawaua Wafilistini wengi na kunyanganya ngombe wengi. Kwa hiyo Daudi aliwaokoa wakaaji wa Keila.


Hata alipomwomba Yawe shauri, Yawe hakumujibu kwa ndoto, kwa mawe ya kupiga kura, wala kwa njia ya manabii.


Daudi akamwomba Yawe shauri: “Nikifuata kundi hili nitalikamata?” Yawe akamujibu: “Ulifuate maana utalipata na kuwaokoa hao waliotekwa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ