28 Kwa hiyo, Saulo akaacha kumufuatilia Daudi, akaenda kupigana na Wafilistini. Ndiyo maana pahali pale pakaitwa “Jiwe la Matengano.”
Tumeponyoka kama ndege katika mutego; mutego umefyatuka, nasi tukaponyoka.
Saulo na watu wake wakaanza kumutafuta Daudi. Lakini Daudi alipopata habari zile, alikwenda kujificha kwenye mawe makubwa, yanayokuwa katika mbuga za Maoni na kukaa kule. Saulo aliposikia habari zile, alimufuatilia Daudi kule kwenye mbuga za Maoni.
Hapo mutu mumoja akamwendea Saulo na kumwambia: “Kuja haraka; Wafilistini wanaishambulia inchi.”
Daudi aliondoka pahali pale, akaenda kuishi kwenye makimbilio ya muji wa Engedi.
Saulo aliporudi kutoka kupigana na Wafilistini, alipata habari kwamba Daudi yuko kwenye mbuga za Engedi.