1 Samweli 23:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
24 Basi, wakaondoka kwenda Zifu, wakimutangulia Saulo. Wakati ule, Daudi na watu wake walikuwa katika mbuga za Maoni, katika bonde la Araba upande wa kusini wa jangwa.
Muchunguze kila upande mujue pahali anapojificha, kisha muniletee habari kamili. Halafu nitakwenda pamoja nanyi na ikiwa angali kule, basi, mimi nitamutafuta kati ya maelfu yote ya watu wa Yuda.”
Saulo na watu wake wakaanza kumutafuta Daudi. Lakini Daudi alipopata habari zile, alikwenda kujificha kwenye mawe makubwa, yanayokuwa katika mbuga za Maoni na kukaa kule. Saulo aliposikia habari zile, alimufuatilia Daudi kule kwenye mbuga za Maoni.
Kulikuwa mutu mumoja kule katika muji wa Maoni ambaye alikuwa na biashara ya kondoo katika muji wa Karmeli. Kule Karmeli alifuga kondoo wake na kuwakata manyoya. Alikuwa tajiri sana. Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja.