Hakuna kitu kinachoweza kufichwa mbele ya Mungu, lakini vitu vyote vinafunuliwa na viko wazi mbele ya macho yake, yeye tutakayemutolea hesabu ya maneno yetu.
Wakaaji wa Keila watanitia katika mikono ya Saulo? Saulo atakuja kweli kama nilivyosikia mimi mutumishi wako? Ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakuomba unijibu mimi mutumishi wako.” Yawe akamujibu: “Saulo atakuja.”
Saulo alipoambiwa kwamba Daudi amekwisha fika Keila, akasema: “Mungu amemutia katika mikono yangu maana amejifungia mwenyewe kwa kuingia katika muji wenye milango yenye vifungio.”