Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 22:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Siku moja, Saulo alikuwa Gibea, akiikaa chini ya muti wa mukwaju, kwenye mulima, naye alikuwa na mukuki wake katika mukono na watumishi wake walikuwa wakimuzunguka. Basi akaambiwa kwamba Daudi na watu wake wameonekana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 22:6
7 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abrahamu akapanda muti wa mukwaju kule Beri-Seba, akaomba kwa jina la Yawe, akamwabudu Mungu, Mungu wa milele.


Debora alikuwa anazoea kuikaa chini ya muti wa ngazi uliokuwa kati ya muji wa Rama na muji wa Beteli katika inchi ya milima ya Efuraimu. Watu wa Israeli walimufikia kusudi awaamulie mashauri yao.


Saulo alikuwa amepiga kambi chini ya muti wa mukomamanga kule Migroni, inje ya muji wa Gibea, akiwa pamoja na watu yapata mia sita.


Kesho yake, pepo muchafu kutoka kwa Mungu akamushambulia Saulo kwa rafla, akakuwa anapayukapayuka kama mwenda-wazimu katika nyumba yake. Daudi alikuwa anapiga kinubi kama alivyofanya siku zote. Saulo alikuwa na mukuki katika mukono wake.


Halafu, pepo muchafu kutoka kwa Yawe akamushika Saulo alipokuwa akiikaa ndani ya nyumba yake, akishika mukuki katika mukono, wakati Daudi alikuwa akipiga kinubi.


Lakini Saulo akamutupia Yonatani mikuki kusudi amwue. Naye Yonatani akatambua kwamba baba yake alikuwa amekusudia kumwua Daudi.


Kisha, wakaitwaa mifupa yao na kuizika chini ya muti wa mukwaju kule Yabesi, nao wakafunga kula chakula kwa muda wa siku saba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ