Kisha aliwashinda Wamoabu. Aliwapanga katika mistari mateka hao, na kuwalalisha chini. Aliamuru wale waliokuwa katika mistari miwili wauawe na wale wa mustari wa tatu waachwe wazima. Hivyo, Wamoabu wakakuwa watumishi wa Daudi na wakakuwa wanamulipa kodi.
Hawa ndio watu waliovuka muto Yordani katika mwezi wa kwanza, muto ulipokuwa umefurika pande zote na kuwatawanya watu kwa upande wa mashariki na magaribi ya muto.
Habari za mufalme Daudi toka mwanzo mpaka mwisho juu ya mambo ya utawala wake, uwezo wake, na mambo yaliyomupata yeye, Waisraeli, na falme zote katika inchi zimeandikwa katika vitabu vya nabii Samweli, katika vitabu vya nabii Natani, vilevile katika vitabu vya nabii Gadi.
Mufalme Hezekia alifuata maagizo ambayo Yawe alikuwa amemupa mufalme Daudi kwa njia ya Gadi, nabii wa mufalme na nabii Natani. Hivyo basi, akaweka Walawi katika nyumba ya Yawe, wamoja wao wakiwa na matoazi, wengine vinanda na wengine vinubi. Hiyo ilikuwa amri ya Yawe kwa njia ya manabii wake.
Lakini mimi nikajiuliza ndani ya moyo: “Mutu kama mimi ataweza kukimbia? Mutu kama mimi anahitaji kuingia katika hekalu apate kuponyesha maisha yake? Sitaingia hata kidogo katika hekalu.”
Watakapowatesa katika muji mumoja, mukimbilie katika muji mwingine. Kweli ninawaambia: hamutamaliza kuzunguka katika miji yote ya Israeli mbele ya kurudi kwa Mwana wa Mutu.
Kutoka kule, Daudi alikwenda mpaka Misipa katika inchi ya Moabu. Akamwambia mufalme wa Moabu: “Tafazali, baba yangu na mama yangu wakae hapa kwako mpaka nijue Mungu atanifanyia nini.”
Kisha nabii Gadi akamwambia Daudi: “Usikae hapa katika makimbilio. Ondoka mara moja uende katika inchi ya Yuda.” Basi, Daudi akaondoka, akaenda katika pori la Hereti.