Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 22:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kutoka kule, Daudi alikwenda mpaka Misipa katika inchi ya Moabu. Akamwambia mufalme wa Moabu: “Tafazali, baba yangu na mama yangu wakae hapa kwako mpaka nijue Mungu atanifanyia nini.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 22:3
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yosefu akawapa baba yake na wandugu zake eneo la Ramesesi lililokuwa bora kabisa katika inchi ya Misri, likuwe makao yao, nao wakalirizi kama vile mufalme alivyoagiza.


Kisha aliwashinda Wamoabu. Aliwapanga katika mistari mateka hao, na kuwalalisha chini. Aliamuru wale waliokuwa katika mistari miwili wauawe na wale wa mustari wa tatu waachwe wazima. Hivyo, Wamoabu wakakuwa watumishi wa Daudi na wakakuwa wanamulipa kodi.


Uwaheshimu baba yako na mama yako, kusudi uishi maisha marefu katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Lakini kama mujane akiwa na watoto au wajukuu, inafaa wajifunze kwanza kutimiza mapaswa yao ya kidini kwa ajili ya jamaa zao wenyewe na kuwarudishia wazazi na babu zao mema waliyowatendea, kwa maana jambo hilo linamupendeza Mungu.


Kisha roho wa Yawe akamujaza Yefuta, naye akaondoka na kupitia Gileadi na Manase, akarudi Misipa katika inchi ya Gileadi na kuendelea mpaka Amoni.


Zaidi ya hayo, nimemupata Ruta wa Moabu mujane wa Malona, kusudi akuwe muke wangu. Mapatano haya yatafanya mali ya jamaa ya marehemu na ukoo wake kubakia kwa watu wake katika muji huu. Ninyi ni washuhuda.”


Wanawake wajirani wakatangaza jina wakisema: “Mutoto amezaliwa kwa Naomi”, nao wakamwita jina la Obedi. Kisha Obedi akamuzaa Yese aliyemuzaa Daudi.


Saulo alipokwisha kuwa mufalme wa Waisraeli, alipigana na waadui zake wote kila upande: Wamoabu, Waamoni, Waedomu, wafalme wa Zoba na Wafilistini. Kila mara alipopigana vita, alishinda.


Watu wote waliogandamizwa au waliokuwa na madeni au wale wenye huzuni walijiunga na Daudi. Jumla yao ilikuwa watu yapata mia ine, naye akakuwa kiongozi wao.


Basi, Daudi aliwaacha wazazi wake wakae na mufalme wa Moabu; nao wakakaa kwake kwa muda wote ambao Daudi alikuwa katika nafasi za makimbilio.


Basi, Samweli akamwelezea Eli yote aliyoambiwa, bila kumuficha chochote. Halafu Eli akasema: “Yeye ni Yawe; afanye anachoona ni chema kwake.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ