Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 21:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kwa hiyo kuhani Ahimeleki akamupa mikate mitakatifu, maana hapakukuwa mikate mingine isipokuwa ile ambayo inaondolewa mbele ya Yawe na kubadilishwa na mikate mipya kutoka kwenye jiko.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 21:7
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

wachungaji wa pale Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaka wakisema: “Maji haya ni yetu.” Hivyo Isaka akakiita kisima hicho “Ugomvi” kwa sababu waligombana naye.


Hata katika jangwa vilevile alijenga minara, akachimba visima vingi, maana alikuwa na makundi mengi ya nyama kwenye sehemu za miinuko na mabonde. Alikuwa na walimaji na watunza mizabibu kwenye milima, na katika inchi yenye mboleo maana alipenda mulimo.


Basi, wanakuja kwako makundi kwa makundi na kuikaa mbele yako kama watu wangu, kusudi wasikie unachosema, lakini hawafanyi unachowaambia wafanye. Wanasema kwamba wana upendo, lakini hayo ni kusema tu; wanachotafuta kwa moyo ni faida yao tu.


Mutu asiyekuwa wa ukoo wa makuhani haruhusiwi kula chakula kitakatifu. Hata mugeni wa kuhani au mutumishi wake haruhusiwi kula.


Lakini kama binti ya kuhani ni mujane au amefukuzwa na mume wake na hana mutoto, naye amerudi kwa baba yake na kukaa naye kama vile alipokuwa kijana, basi, anaweza kula chakula cha baba yake. Hata hivyo, mugeni haruhusiwi kula chakula hicho.


Twaa unga laini, kilo kumi na mbili na kupika mikate kumi na miwili.


Kila siku ya Sabato Haruni ataipanga sawasawa katika mustari mbele yangu mimi Yawe kwa ajili ya watu wa Israeli kama vile agano la milele.


Munajisemesha ndani ya mioyo yenu: Sikukuu ya mwandamo wa mwezi itakwisha wakati gani kusudi tuanze tena kuuzisha vyakula vyetu? Siku ya Sabato itakwisha wakati gani kusudi tupate kuuzisha ngano yetu? Tutapunguza vipimo, tutapandisha bei, tutadanganya watu kwa mizani zisizokuwa sawa.


‘Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao. Lakini mioyo yao ni mbali nami.


Sasa, Saulo alikuwa anatoka kwenye shamba akiwa na ngombe dume wake, akauliza: “Watu wana nini? Kwa nini wanalia?” Wakamwambia habari wajumbe waliyoleta kutoka Yabesi.


Saulo alipokwisha kuwa mufalme wa Waisraeli, alipigana na waadui zake wote kila upande: Wamoabu, Waamoni, Waedomu, wafalme wa Zoba na Wafilistini. Kila mara alipopigana vita, alishinda.


Basi siku ile pale kulikuwa mutumishi mumoja wa Saulo ambaye alikuwa amezuiliwa mbele ya Yawe. Mutumishi yule aliitwa Doegi Mwedomu, aliyekuwa musimamizi wa wachungaji wa nyama wa Saulo.


Ahimeleki alimwombea Daudi kwa Yawe, akamupa chakula na upanga wa yule Mufilistini Goliati.”


Naye Daudi akamwambia Abiatari: “Nilijua wazi siku ile nilipomwona Doegi Mwedomu, kwamba atamwambia Saulo. Kwa hiyo mimi nimesababisha vifo vya watu wa jamaa ya baba yako.


Kwa hiyo Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa amesimama karibu na watumishi wa Saulo akasema: “Nilimwona mwana wa Yese alipofika Noba kwa kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ