Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 21:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kuhani Ahimeleki akamwambia: “Hapa sina mukate wa kawaida. Niko tu na ile mikate mitakatifu. Munaweza kupewa mikate hiyo ikiwa watu wako wamejitenga na wanawake siku hizi.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 21:5
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Musa akashuka toka juu ya mulima na kuwaendea watu, akawatakasa, nao wakafua nguo zao.


Kisha akawaambia watu wote: “Kesho kutwa mukuwe tayari na mwanaume yeyote asimukaribie mwanamuke.”


Meza hiyo utaiweka mbele ya Sanduku la Agano na juu ya meza ile utaweka ile mikate muliyonitolea. Mikate ile itakuwa siku zote mbele yangu.


Haruni na wazao wake peke yao ndio wanaoruhusiwa kula mikate hiyo maana ni mitakatifu kabisa kwa sababu ni sehemu ya sadaka ninazotolewa mimi Yawe kwa moto. Hiyo ni haki yao milele.


Kisha, kwenye kile kitunga cha mikate iliyowekwa mbele ya Yawe akatwaa mukate mumoja usiotiwa chachu, mukate mumoja wenye mafuta na mukate mumoja mudogo, akaviweka vyote juu ya vipande vya mafuta na ule muguu.


Lakini Bwana akamwambia: “Kwenda tu, kwa maana nimemuchagua mutu huyu kwa kunitumikia, kusudi atangaze jina langu kwa mataifa, kwa wafalme na kwa Waisraeli.


Musinyimane, isipokuwa tu mumepatana na kwa muda tu kusudi mupate wakati wa kujitoa kwa kufunga na kuomba. Kisha munaweza kurudiliana tena kusudi Shetani asiwajaribu katika uzaifu wenu.


Kwa maana kuteswa kwa ajili ya kutenda mema, ikiwa ni mapenzi ya Mungu, ni vizuri kuliko kuteswa kwa ajili ya kutenda mabaya.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ