na kuwauliza makuhani wa hekalu la Yawe wa majeshi maneno haya: Tuendelee kuomboleza na kufunga kula chakula katika mwezi wa tano kama tulivyofanya kwa muda wa miaka mingi sasa?
Musinyimane, isipokuwa tu mumepatana na kwa muda tu kusudi mupate wakati wa kujitoa kwa kufunga na kuomba. Kisha munaweza kurudiliana tena kusudi Shetani asiwajaribu katika uzaifu wenu.
Daudi akamujibu: “Niko hapa kutokana na amri ya mufalme. Aliniambia nisimwelezee mutu yeyote juu ya kile ambacho amenituma. Nimeagana na watu wangu kwamba tukutane pahali fulani.
Daudi akamwambia: “Kwa hakika, ninapokwenda kwa ajili ya shuguli kubwa, wanawake wanatengwa mbali nasi! Ikiwa miili ya vijana wangu inakuwa mitakatifu na safi tunapokuwa kwenye shuguli za kawaida, basi, si zaidi katika shuguli hii kubwa?”