Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 21:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Daudi alikwenda kwa kuhani Ahimeleki kule Noba. Ahimeleki akaenda kumupokea akiwa anatetemeka, akamwuliza: “Kwa nini umekuja hapa peke yako?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 21:2
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Isaka akamwuliza: “Imekuwa namna gani hata umepata mawindo upesi hivyo, mwana wangu?” Yakobo akamujibu: “Yawe, Mungu wako, amenifanikisha.”


Akamwuliza tena: “Kweli wewe ndiwe mwana wangu Esau?” Naye akamujibu: “Ndiyo.”


Yule muzee wa Beteli akamwambia: “Mimi vilevile ni nabii kama wewe, na Yawe amesema nami kwa njia ya malaika akisema: ‘Umurudishe kwako, akule chakula na kunywa maji.’ ” Lakini yule nabii muzee alikuwa anamudanganya tu.


Uniepushe na njia za upotovu; unifundishe kwa huruma sheria yako.


Ee Yawe, ulinde kinywa changu, uweke mulinzi kwenye mulango wa kinywa changu.


Leo hii, adui atapiga kambi kule Noba, anainua mukono wake kwa mulima Sayuni, kilima cha Yerusalema.


Kwa maana mbele ya kufika kwa watu wamoja waliotumwa na Yakobo kule, yeye alizoea kula pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini watu wale walipofika, akajitenga na kuacha kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa sababu ya kuogopa wale wanaolazimisha kutahiriwa.


Musiambiane uongo ninyi kwa ninyi, kwa maana mumeondoa utu wenu wa zamani pamoja na matendo yake


Halafu Saulo akamwuliza Mikali: “Kwa nini umenidanganya? Umemwacha adui yangu atoroke?” Naye Mikali akamujibu Saulo: “Aliniambia: ‘Uniache niende kusudi nisipate kukuua.’ ”


Daudi akamujibu: “Niko hapa kutokana na amri ya mufalme. Aliniambia nisimwelezee mutu yeyote juu ya kile ambacho amenituma. Nimeagana na watu wangu kwamba tukutane pahali fulani.


Naye Daudi akamwambia Abiatari: “Nilijua wazi siku ile nilipomwona Doegi Mwedomu, kwamba atamwambia Saulo. Kwa hiyo mimi nimesababisha vifo vya watu wa jamaa ya baba yako.


Kwa hiyo Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa amesimama karibu na watumishi wa Saulo akasema: “Nilimwona mwana wa Yese alipofika Noba kwa kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ