Yule muzee wa Beteli akamwambia: “Mimi vilevile ni nabii kama wewe, na Yawe amesema nami kwa njia ya malaika akisema: ‘Umurudishe kwako, akule chakula na kunywa maji.’ ” Lakini yule nabii muzee alikuwa anamudanganya tu.
Kwa maana mbele ya kufika kwa watu wamoja waliotumwa na Yakobo kule, yeye alizoea kula pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini watu wale walipofika, akajitenga na kuacha kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa sababu ya kuogopa wale wanaolazimisha kutahiriwa.
Daudi akamujibu: “Niko hapa kutokana na amri ya mufalme. Aliniambia nisimwelezee mutu yeyote juu ya kile ambacho amenituma. Nimeagana na watu wangu kwamba tukutane pahali fulani.
Naye Daudi akamwambia Abiatari: “Nilijua wazi siku ile nilipomwona Doegi Mwedomu, kwamba atamwambia Saulo. Kwa hiyo mimi nimesababisha vifo vya watu wa jamaa ya baba yako.
Kwa hiyo Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa amesimama karibu na watumishi wa Saulo akasema: “Nilimwona mwana wa Yese alipofika Noba kwa kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu.