Nitamutuma mutumishi wangu aende kuitafuta mishale hiyo. Kama nikimwambia: ‘Angalia, mishale hiyo iko upande ule wako, uikamate’, hiyo itakuwa na maana kwamba uko salama, nawe utajitokeza kutoka pahali ulipojificha, maana, kama vile Yawe anavyoishi, kuna amani kwako, na hakuna hatari.
Halafu Yonatani akamwambia Daudi: “Uende na amani. Tumekwisha wote kuapa kwa jina la Yawe kwamba Yawe akuwe mushuhuda kati yetu milele, na kati ya wazao wangu na wazao wako milele.”