Tena, kesho kutwa, watu watakukosa kabisa. Siku hiyo uende pahali ambapo ulijificha wakati jambo hili lilipokuwa lingali motomoto, ujifiche nyuma ya lundo la mawe.
Nitamutuma mutumishi wangu aende kuitafuta mishale hiyo. Kama nikimwambia: ‘Angalia, mishale hiyo iko upande ule wako, uikamate’, hiyo itakuwa na maana kwamba uko salama, nawe utajitokeza kutoka pahali ulipojificha, maana, kama vile Yawe anavyoishi, kuna amani kwako, na hakuna hatari.