Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 20:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yonatani akamujibu: “Jambo hilo lipite mbali nawe. Hautakufa. Baba yangu hafanyi jambo lolote, likuwe kubwa au dogo, bila kunielezea. Hata jambo hili hawezi kunificha. Sivyo inavyokuwa hata kidogo.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 20:2
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wao wakamwuliza: “Bwana, una maana gani kutuambia maneno kama hayo? Sisi watumishi wako hatuwezi kufanya jambo kama hilo!


Ee Yawe, Mungu wangu, umetufanyia maajabu mengi, na mipango yako juu yetu haihesabiki; hakuna yeyote anayekuwa kama wewe. Kama ningeweza kusimulia hayo yote, hesabu yake ingenishinda.


Anayeshirikiana na mwizi anajizuru mwenyewe; anasikia laana ikitolewa bila kusema neno.


Bwana wetu Yawe amenifanya kuwa musikilivu, nami sikukataa wala kurudia nyuma.


Atakuja na kuwaua wale walimaji. Na kisha atawapatia walimaji wengine shamba lile.” Watu waliposikia maneno hayo, wakasema: “Isitufikie vile hata kidogo.”


Siwaiti ninyi tena watumishi, kwa sababu mutumishi hajui mambo bwana wake anayofanya. Ninawaita ninyi warafiki kwa sababu nimewajulisha yote niliyosikia kutoka kwa Baba yangu.


kwa maana nimewatangazia maneno yale uliyoniagiza, nao wameyakubali. Wamejua hakika kwamba nilitoka kwako na kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Sisi hatukuwa na nia ya kumwasi sasa Yawe hata kidogo na kumwacha kwa kujenga mazabahu ya kutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto au sadaka za unga au sadaka zingine. Hatupendi kutolea sadaka pahali pengine isipokuwa juu ya mazabahu ya Yawe, Mungu wetu, inayokuwa katika makao yake.”


Halafu watu wakamujibu: “Hatutaweza hata kidogo kumwacha Yawe na kuitumikia miungu mingine.


Lakini watu wakamwambia Saulo: “Kwa nini Yonatani, aliyeletea Waisraeli ushindi huu mukubwa, auawe? Haiwezikani hata kidogo. Kama vile Yawe anavyoishi, hata unywele mumoja wa kichwa chake hautaanguka chini. Alichokifanya leo, amekifanya kwa musaada wa Yawe.” Kwa hiyo, watu walimukomboa Yonatani naye hakuuawa.


Daudi alikimbia kutoka Nayoti katika Rama, akaenda mpaka kwa Yonatani, akamwambia: “Nimefanya nini? Kosa langu ni gani? Nimemutendea baba yako zambi gani hata anajaribu kuyaangamiza maisha yangu?”


Yonatani akamwambia Daudi: “Yawe, Mungu wa Israeli, akuwe mushuhuda kati yetu. Kesho au kesho kutwa, wakati kama huu nitamwuliza baba yangu. Ikiwa musimamo wake juu yako ni muzuri nitakuelezea.


Daudi akaapa vilevile: “Hakika baba yako anajua vizuri kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako. Anafikiri kukuficha juu ya jambo hili kusudi usihuzunike atakapolitenda. Lakini kweli, kama Yawe anavyoishi na kama wewe mwenyewe unavyoishi, kati yangu na lufu kuna hatua moja tu!”


Jana yake, mbele ya Saulo kufika katika muji pale, Yawe alikuwa amemwambia Samweli hivi:


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ