Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 20:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Yawe aniue ikiwa Saulo anakusudia kukuzuru nami nisipokujulisha kusudi uende pahali pa mbali ambapo utakuwa salama. Yawe akuwe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 20:13
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninyi ni wandugu zangu, ninyi ni damu yangu. Kwa nini mukuwe wa mwisho kunirudisha mimi mufalme kwangu?


Kisha, watu wote walikwenda kumusihi Daudi akule chakula wakati ulipokuwa bado muchana. Lakini Daudi aliapa akawaambia: “Mungu aniue ikiwa nitaonja chakula au kitu chochote mpaka jua litakapotua.”


Lakini sitaacha kumutendea mema yangu kama vile nilivyoacha kwa Saulo, niliyemwondoa mbele yako.


Kama Yawe alivyokuwa pamoja na bwana wangu mufalme, akuwe vilevile na Solomono, na akitukuze kiti chake cha kifalme kuliko kiti cha kifalme cha bwana wangu mufalme Daudi.”


Yezebeli akatuma mujumbe kwa Elia amwambie: “Miungu waniue, ninakuapia, kama kesho nisipokuua kwa wakati kama huu sawa vile ulivyowaua wale manabii.”


Beni-Hadadi akamutumia Ahabu ujumbe huu: “Miungu iniue ikiwa kule Samaria kutabakia mavumbi ya kutosha kwa kujaza vitanga vya mikono kwa kila mumoja wa watu wangu wengi wanaonifuata!”


“Sasa, mwana wangu, Yawe, Mungu wako, akuwe pamoja nawe kusudi uweze kumujengea nyumba kama vile alivyosema.


wa kufua zahabu, feza, shaba na chuma. Basi sasa, anza kazi! Yawe akuwe pamoja nawe!”


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Mushike mambo yote muliyojifunza na kupokea toka kwangu, nayo yote muliyosikia na kuona kwangu. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.


Hakuna mutu atakayekushinda siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Musa. Siku zote nitakuwa nawe wala sitakuacha hata kidogo.


Pale utakapokufia ni pale nitakufia nami, na ni palepale nitazikwa. Yawe anipe azabu kali kama nikitenganishwa nawe isipokuwa tu kwa kifo.”


Wakati mambo haya yatakapokutokea, chochote utakachoweza kufanya ukifanye, maana Mungu yuko pamoja nawe.


Saulo alipokwisha kuwa mufalme wa Waisraeli, alipigana na waadui zake wote kila upande: Wamoabu, Waamoni, Waedomu, wafalme wa Zoba na Wafilistini. Kila mara alipopigana vita, alishinda.


Yawe ambaye ameniokoa toka katika makucha ya simba na dubu, ataniokoa kutoka kwa Mufilistini huyu.” Saulo akamwambia: “Kwenda, naye Yawe akuwe pamoja nawe.”


Saulo alikuwa anamwogopa Daudi kwa sababu Yawe alikuwa pamoja naye, lakini Yawe alikuwa amemwacha Saulo.


Mimi nitakuja na kusimama karibu na baba yangu kule katika shamba pahali utakapokuwa. Pale nitaongea naye juu yako, na kitu chochote nitakachogundua kutoka kwake, nitakuelezea.”


Yonatani akamwambia Daudi: “Yawe, Mungu wa Israeli, akuwe mushuhuda kati yetu. Kesho au kesho kutwa, wakati kama huu nitamwuliza baba yangu. Ikiwa musimamo wake juu yako ni muzuri nitakuelezea.


Ikiwa nitaendelea kuishi basi, unionyeshe wema wa Yawe, kusudi nisikufe,


Mungu aniue mimi ikiwa kesho asubui nitakuwa sijawaua wanaume wake wote.”


Eli akamwuliza: “Yawe alikuambia nini? Usinifiche alichokuambia. Ikiwa utanificha kitu alichokuambia, Mungu akuazibu vikali.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ