11 Yonatani akamujibu: “Kuja tuende ndani ya shamba!” Basi, wakaenda.
Daudi akauliza: “Nitajua namna gani ikiwa baba yako atakujibu kwa ukali?”
Yonatani akamwambia Daudi: “Yawe, Mungu wa Israeli, akuwe mushuhuda kati yetu. Kesho au kesho kutwa, wakati kama huu nitamwuliza baba yangu. Ikiwa musimamo wake juu yako ni muzuri nitakuelezea.