Yosefu alipoona kaka zake akawatambua, lakini akajifanya sawa vile hawafahamu, akasema nao kwa ukali. Akawauliza: “Mumetoka wapi ninyi?” Wakamujibu: “Tumetoka katika inchi ya Kanana, tumekuja kununua chakula.”
Kijana mumoja wa Nabali, akamwambia Abigaili, muke wa Nabali: “Daudi alituma wajumbe toka katika jangwa kuja kumusalimia bwana wetu. Lakini yeye aliwatukana.
Sasa ufikiri juu ya jambo hili na uamue la kufanya. Jambo hili linaweza kuleta hasara kwa bwana wetu na jamaa yake yote. Yeye ni mutu mubaya na hakuna anayeweza kusema naye.”