Basi, haya ndiyo niliyotambua: jambo zuri na lenye kufaa kwa mwanadamu ni kula, kunywa na kufurahia matunda ya jasho anayotoa hapa chini ya jua, siku zile chache za maisha aliyojaliwa na Mungu, maana hivi ndivyo alivyopangiwa.
Tena, nimeona kitu kimoja hapa chini ya jua, kwamba wenye kukimbia mbio hawashindi katika mashindano ya kukimbia, wala wenye nguvu hawashindi vita, wenye hekima hawapati chakula, wenye akili hawatajiriki, wala wenye ujuzi hawapandi vyeo. Lakini wakati wa bahati unawapata wote pamoja.
Watu wanauliza: Kwa nini sisi tunakaa tu hapa? Tukusanyike, tuingie katika miji yenye kuzungukwa na kuta, tuangamie kule! Yawe, Mungu wetu, amekusudia tuangamie, ametupa maji yenye sumu tukunywe, kwa sababu tumemukosea yeye.
Anayetaka kujivuna, ajivune kwamba ananifahamu mimi, kwamba anajua kwamba mimi Yawe ninatenda mema, ninafanya mambo ya haki kufuatana na sheria yangu katika dunia. Watu wa namna hiyo ndio wanaonipendeza. –Ni ujumbe wa Yawe.
Siku hiyo itakuwa siku ya kasirani, ni siku ya taabu na uchungu, siku ya giza na huzuni; siku ya uharibifu na maangamizi, siku ya mawingu na giza kubwa.
Yule malaika akaniambia vilevile niseme neno hili la Yawe juu ya Zerubabeli: Hauwezi kushinda kwa nguvu au kwa uwezo wako mwenyewe, lakini kwa musaada wa roho wangu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema.
Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.
Wale walimu wa uongo ni kama visima visivyokuwa na maji tena, wao ni kama mawingu yanayopeperushwa na upepo; makao yao yametayarishwa kwenye giza nzito.
Barua hii inatoka kwangu mimi Yuda, mutumishi wa Yesu Kristo na ndugu wa Yakobo. Ninawaandikia ninyi mulioitwa na Mungu Baba na munaoishi katika upendo wake na kulindwa kwa ajili ya Yesu Kristo.
Wanafanana na zoruba kubwa ya bahari na matendo yao ya haya yanaonekana kama pofu ya zoruba. Wanafanana vilevile na nyota zinazotangatanga; Mungu amekwisha kuwawekea nafasi katika giza kubwa kwa milele.
Wapendwa wangu, wakati nilipokuwa nikifanya bidii sana ya kuwaandikia juu ya wokovu tunaoshiriki wote pamoja, nikaona sherti niwaandikie na kuwaonya mupate kutetea imani ile Mungu aliyotoa mara moja tu kwa watu wake.
Sasa bwana wangu, kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, unaona kwamba Yawe amekuzuia kulipiza kisasi kwa kumwanga damu na hivyo upate kuwa na kosa. Uwaache waadui zako na wale wote wanaokutakia mabaya wakuwe wapumbafu kama Nabali.