Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Anawainua wazaifu toka katika mavumbi, anawanyanyua wakosefu toka katika majivu, na kuwaikalisha pamoja na wakubwa, na kuwarizisha viti vya heshima. Maana, minara ya dunia ni ya Yawe; yeye ameisimika dunia juu ya minara yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 2:8
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, mufalme akaamuru Yosefu aitwe; naye akaondolewa katika kifungo haraka. Kisha kunyoa na kubadilisha nguo zake, Yosefu akakuja mbele yake.


Wewe ndiwe utakayeisimamia inchi yangu, na watu wangu wote watakuwa chini ya amri yako. Mimi tu ndiye mukubwa kuliko wewe kwa kuwa ninaikalia kiti cha kifalme.


Kwa hiyo basi, umwambie mutumishi wangu Daudi: Yawe wa majeshi anasema hivi: Nilikutoa katika shamba la malisho ya nyama ulimokuwa unawachunga kondoo, kusudi ukuwe mukubwa wa watu wangu Waisraeli.


“Wewe Basha, mimi nilikuinua kutoka katika mavumbi, nikakufanya kiongozi wa watu wangu Waisraeli. Wewe umefuata mwenendo wa Yeroboamu. Uliwasukuma watu wangu Waisraeli watende zambi na kunikasirikisha kwa zambi zao.


Halafu wote wawili wakaingia ndani ya chumba cha ndani na kule nabii akamutia Yehu mafuta juu ya kichwa na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Ninakupakaa mafuta ukuwe mufalme juu ya watu wangu Israeli.


akisema: Nilikuja uchi katika dunia, nitaondoka uchi katika dunia. Yawe amenipa, Yawe ametwaa. Jina la Yawe litukuzwe.


Yobu akatwaa kigae, akajikuna nacho na kuikaa kwenye majivu.


Ee Mungu wangu, usinihamishe sasa wakati ningali bado kijana. Ee Yawe, wewe unadumu milele.


Umeiweka dunia imara juu ya misingi yake, isitikisike hata milele.


Lakini aliwaokoa wakosefu katika taabu zao, akaongeza jamaa zao kama kundi la kondoo.


Maana yeye aliweka misingi ya dunia juu ya bahari; aliisimika imara juu ya maji mengi.


Mungu anasema: “Mimi nimeweka wakati kamili! Wakati huo nitahukumu kwa haki.


Inchi ikitetemeka na vyote vinavyokuwa ndani yake, mimi ndiye ninayeimarisha misingi yake.


Ukubwa hautoki mashariki au magaribi, wala hautoki katika jangwa au kwa milima.


hata ikiwa alikuwa mufungwa na sasa ni mufalme, au alizaliwa masikini na sasa ni mufalme.


Nitamwimarisha Eliakimu kama musumari uliopigiliwa pahali pagumu, naye atapata heshima tukufu katika ukoo wa wazee wake.


Kisha mufalme Nebukadneza akamupandishia Danieli heshima kubwa, akamupa zawadi nyingi kubwakubwa, na kumufanya kuwa mutawala wa jimbo lote la Babeli, na mukubwa wa wenye hekima wote wa Babeli.


Muti uliouona ukiwa mukubwa na wenye nguvu, ambao matawi yake marefu yalifika mbinguni, nao ukionekana kutoka kila pahali katika dunia,


Aliweka vilevile wakubwa watatu, Danieli akiwa mumoja kati yao, wawasimamie wale wakubwa wengine katika uongozi kusudi mufalme asipatwe na hasara.


Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.


Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.


Hivi akatupatia ufalme wa kikuhani kusudi tumutumikie Mungu Baba yake. Yesu Kristo atukuzwe na kuwa na uwezo kwa milele na milele. Amina.


Hakutakuwa usiku tena, wala hawatakuwa na lazima ya mwangaza wa taa wala jua, kwa sababu Bwana wetu na Mungu wetu mwenyewe atawaangazia, nao watatawala milele na milele.


Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.


Umewapatia ufalme wa kikuhani kusudi wamutumikie Mungu wetu; nao watatawala katika dunia.”


Samweli akamwambia: “Ingawa unajiona kwamba wewe ni mudogo, lakini si wewe kiongozi wa makabila ya Israeli? Yawe alikupakaa mafuta kwa kukusimika kuwa mufalme juu ya Israeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ