Halafu wote wawili wakaingia ndani ya chumba cha ndani na kule nabii akamutia Yehu mafuta juu ya kichwa na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Ninakupakaa mafuta ukuwe mufalme juu ya watu wangu Israeli.
Mufalme Hezekia akatajirika sana na kuheshimiwa. Alijitengenezea hazina za feza, za zahabu, za mawe ya bei kali za viungo, ngao na za aina zote za vyombo vya bei kubwa.
Halafu miti yote katika inchi itajua kwamba mimi Yawe ninaishusha miti mirefu na kuinua miti mifupi. Mimi ninakausha miti mibichi na kustawisha miti yenye kukauka. Ni mimi Yawe ninayesema hayo na nitayafanya.