Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 2:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yawe anaua na kufufua, yeye anawashusha katika kuzimu naye anawarudisha tena.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 2:6
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akasikiliza ombi la Elia. Mutoto akaanza kupumua tena.


Mufalme wa Israeli aliposoma barua hii alipasua nguo yake na kusema: “Sababu gani mufalme wa Aramu anataka nimuponyeshe mutu huyu ukoma wake? Anafikiri kwamba mimi ni Mungu anayekuwa na uwezo wa kuua au kufufua? Mufahamu basi, muone kwamba mutu huyu anataka kuniletea ugomvi!”


Maana yeye anaumiza na tena anatunza, anatia kidonda na kwa mukono wake anaponyesha.


Hatari ya kifo ilinizunguka, vitisho vya kaburi vilinishika; nilisongwa na mahangaiko na huzuni.


Ee Yawe, umeniokoa kutoka kuzimu; umenipa tena uzima, umenitoa kutoka kati ya wafu.


Yawe asifiwe siku kwa siku! Yeye anatubebea mizigo yetu, yeye ndiye Mungu mwokozi wetu.


Umeniletea taabu kubwa, lakini utanirudishia tena uzima, wewe utaniinua tena kutoka katika shimo.


wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha, wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga,


Wafu wako wataishi tena, miili yao itafufuka. Wanaolala katika mavumbi wataamuka na kuimba kwa furaha! Mungu atapeleka umande wake wa uzima, nao wanaokuwa kwa wafu watatoka wazima.


Kwa hiyo, toa unabii, uwaambie kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Enyi watu wangu, nitayafunua makaburi yenu na kuwafufua kutoka ndani ya makaburi yenu. Nitawarudisha ndani ya nyumba zenu katika inchi ya Israeli.


Yawe akaniuliza hivi: Wewe mwanadamu! Mifupa hii inaweza kuishi tena? Nami nikamujibu: Ee Bwana wetu Yawe, wewe unajua!


Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.


Yesu akamwambia: “Mimi ni ufufuko na uzima, kwa maana anayeniamini, ataishi tena hata ikiwa amekufa.


Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.


Mimi ni mwenye uzima. Nilikuwa nimekufa, lakini sasa mimi niko muzima kwa milele na milele. Niko na mamlaka juu ya lufu na kuzimu.


Daudi akaapa vilevile: “Hakika baba yako anajua vizuri kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako. Anafikiri kukuficha juu ya jambo hili kusudi usihuzunike atakapolitenda. Lakini kweli, kama Yawe anavyoishi na kama wewe mwenyewe unavyoishi, kati yangu na lufu kuna hatua moja tu!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ