Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 2:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Wale ambao zamani walikuwa na chakula tele, sasa wanafanya kazi wapate chakula. Lakini waliokuwa na njaa, sasa hawana njaa tena. Mwanamuke tasa, amezaa watoto saba. Lakini mama mwenye watoto wengi, sasa ameachwa bila mutoto.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 2:5
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anamurudishia heshima mwanamuke anayekuwa tasa; anamufurahisha kwa kumujalia watoto. Haleluia!


Mumwabudu Yawe, enyi watakatifu wake, maana wenye kumwabudu hawakosewi kitu.


Inchi inaomboleza na kunyauka; pori ya Lebanoni imekauka, bonde zuri la Saroni limekuwa jangwa, kule Basani na mulima Karmeli majani yote yamekauka.


Yawe anasema hivi: Imba kwa shangwe, ewe unayekuwa tasa, wewe ambaye haujapata kuzaa! Piga kelele na kuimba kwa nguvu, wewe usiyepata kuzaa mutoto. Maana watoto wako wewe uliyeachwa watakuwa wengi kuliko wa yule anayekuwa na mume.


Mama aliyeheshimiwa kwa kuwa na watoto saba, sasa kwa rafla hana kitu. Amezimia na kukata roho, amekufa angali kijana, amefezeheka na kuzarauliwa. Na wale watakaobaki wazima nitawatoa kwa upanga mbele ya waadui zao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Anawatajirisha wenye njaa, lakini amewaacha watajiri mikono mitupu.


Lakini Abrahamu akamujibu: ‘Mutoto wangu, kumbuka kwamba umekwisha kupewa mema yaliyokupasa wakati ulipoishi katika dunia, na Lazaro alipata taabu. Na sasa yeye anatulizwa, lakini wewe unateswa.


Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Ufurahi wewe tasa, ushangilie, upige kelele wewe usiyejua uchungu wa kuzaa. Kwa maana muke aliyeachwa na mume, atakuwa na watoto wengi kuliko yule anayekuwa naye.”


Yeye atakurudishia uzima wako na atakutunza katika uzee wako. Mukwe wako ni wa lazima zaidi kwako kuliko watoto wa kiume saba, maana anakupenda na amekuzalia mujukuu huyu!”


Hivyo Hana akapata mimba, akazaa mutoto wa kiume. Hana akamwita mutoto huyo Samweli, maana alisema: “Nimemwomba kwa Yawe.”


Penina alikuwa akimuchokoza sana Hana kusudi amukasirikishe kwa sababu Yawe hakumujalia Hana watoto.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ