1 Samweli 2:33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
33 Mutu wako ambaye sitamwangamiza kutoka mazabahu yangu atakuwa ameponyoka kusudi nipofushe macho yake, naye atakufa moyo na wazao wake watauawa kifo kibaya.
Ametoa sadaka ya ngombe, ya wana-ngombe wanono, na kondoo wengi, na amewaalika wana wote wa mufalme, kuhani Abiatari, na Yoabu jemadari wa makundi yako ya waaskari, lakini mutumishi wako Solomono hakualikwa.
basi, mimi nitafanya hivi: Nitawapiga kwa kuwaletea hofu kubwa ya rafla, kifua kikubwa na homa itakayowapofusha macho na kuwakondesha. Mutapanda mbegu zenu bila mafanikio maana waadui zenu ndio watakaozikula.
Utakuwa na wasiwasi na utawaonea wenzako wivu kwa zile baraka zote ambazo nitawapa watu wengine wa Israeli, lakini hakuna mutu katika jamaa yako atakayeishi na kuwa muzee.
Kwa hiyo, mufalme Saulo akamwambia Doegi: “Wewe geuka uwaue makuhani.” Doegi Mwedomu akaenda na kuwaua makuhani wote. Siku hiyo, Doegi aliua makuhani makumi nane na watano ambao wanavaa vizibao vya kikuhani vya kitani.