Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 2:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 2:30
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo Yawe akamwambia Solomono: “Kwa kuwa umeamua kufanya hivyo, ukavunja agano langu nawe, na kuasi masharti yangu niliyokupa, hakika nitakunyanganya huo utawala na kumupa mutumishi wako.


Basi, mufalme Solomono akamufukuza Abiatari, asikuwe kuhani wa Yawe. Hivyo likatimia neno alilosema Yawe kule Shilo, juu ya Eli na ukoo wake.


Nikuambie nini zaidi, mimi Daudi mutumishi wako, kwa kunitukuza vile? Wewe unanijua mimi mutumishi wako.


naye akatoka kwenda kukutana na mufalme Asa, akamwambia: “Unisikilize, ee Asa na watu wote wa kabila la Yuda na la Benjamina! Yawe yuko pamoja nanyi, ikiwa mutakuwa pamoja naye. Mukimutafuta, mutamupata, lakini mukimwacha, naye atawaacha.


na kumuzuia. Wakamwambia: “Si kazi yako hata kidogo Uzia, kumufukizia Yawe ubani. Ni makuhani tu wa uzao wa Haruni ambao wametakaswa kwa kufukiza ubani. Ondoka pahali hapa patakatifu. Umemukosea Yawe na hautapata heshima yoyote kutoka kwake.”


Alinileta, akaniweka kwenye nafasi ya usalama; aliniponyesha kwa sababu alipendezwa nami.


Wewe ni mwema kwa wema, mukamilifu kwa wakamilifu,


Anayenitolea shukrani kama sadaka yake, huyo ndiye anayenitukuza; yeyote anayedumu katika njia yangu, huyo ndiye nitakayemwokoa.”


Ee Bwana, unapoinuka, wanatoweka kama ndoto, kama ndoto wakati mutu anapoamuka.


Mungu anasema: “Nitamwokoa yule anayenipenda; nitamulinda anayejua jina langu!


Akiniita, mimi nitamwitikia; akikuwa katika taabu nitakuwa pamoja naye, nitamwokoa na kumupa heshima.


Haruni na wana wake watavaa makapitula hizo kila mara wanapoingia katika hema la mukutano, au wanapokaribia kwenye mazabahu, kufanya kazi za makuhani katika Pahali Patakatifu. Kwa njia hiyo hawataonyesha uchi wao na kuwa na hatari ya kuuawa. Hilo ni sharti la kufuatwa siku zote kwa Haruni na wazao wake.


Utawafunga mikaba katika viuno na kuwavalisha kofia zao. Hivi ndivyo utakavyowatakasa Haruni na wana wake kuwa makuhani. Hao watakuwa makuhani siku zote kwa ajili ya sharti la siku zote.


Mutu anasifiwa kadiri ya hekima yake, lakini mwenye moyo wa mafikiri mabaya anazaruliwa.


Shikamana sana na hekima, nayo itakutukuza; ukiishikilia itakupa heshima.


Ninawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii wananipata.


Bwana anasema: Watu hawa wanakuja kuniabudu kwa maneno tu, lakini mioyo yao iko mbali nami. Wananiheshimu kulingana na desturi ya watu tu, jambo walilojifunza wao wenyewe.


Kwa hiyo nitamwazibu Semaya wa Nehelamu pamoja na wazao wake. Hakuna hata mumoja wa watu wake atakayebaki muzima na kupata kuona mema nitakayowafanyia watu wangu, kwa sababu amesema maneno ya uasi juu ya Yawe. –Ni ujumbe wa Yawe.


Mimi Yawe nitakufanya wewe Edomu kuwa mudogo kuliko mataifa yote. Ulimwengu wote utakuzarau.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitapingana nanyi, enyi wachungaji. Nitawaondoa madaraka ya kuchunga kondoo wangu, wala sitakubali muwachunge tena. Hamutakuwa tena na nafasi ya kufaidika ninyi wenyewe. Nitawaokoa kondoo wangu toka katika makucha yenu, kusudi wasikuwe chakula chenu tena.


Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoto anamuheshimu muzazi wake, na mutumishi anamuheshimu bwana wake. Ikiwa mimi ndiye Baba wenu, mbona munanivunjia heshima? Ikiwa mimi ni bwana wenu, mbona hamuniheshimu? Ninasema hivyo kwa ninyi makuhani munaozarau jina langu. Nanyi munauliza: Sisi tumezarau jina lako namna gani?


Nitawaazibu watoto wenu na ninyi wenyewe kutokana na uovu wenu, na kuzipakaa nyuso zenu mavi ya nyama wenu wa sadaka. Nitawafukuza mbali nami.


lakini kwa muda wa mwezi muzima! Mutaikula mpaka iwatoke ndani ya pua, mpaka muichukie. Yote hayo ni kwa sababu mumemukataa Yawe anayekuwa hapahapa kati yenu, na kulia mbele yake mukisema: Kwa nini tulitoka Misri?


Musichafue inchi ambayo munakaa ndani yake, inchi ambayo mimi ninakaa ndani yake; maana mimi Yawe ninakaa kati yenu Waisraeli.


Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.


kusudi watu wote wamuheshimu Mwana kama vile wanavyomuheshimu Baba. Asiyemuheshimu Mwana, hamuheshimu Baba aliyemutuma.


Basi namna gani mutaweza kuamini, ninyi munaopokea sifa kutoka wamoja kwa wengine, lakini hamutafuti sifa inayotoka kwake anayekuwa Mungu peke yake?


Yesu akajibu: “Mimi sina pepo, lakini ninamuheshimu Baba yangu, nanyi munanikosea heshima.


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Majaribu hayo ni kwa ajili ya kupima imani yenu. Zahabu ni kitu kinachoharibika, lakini ingawa vile inapimwa kwa njia ya kuchomwa ndani ya moto. Hivi vilevile imani yenu inayokuwa ya bei kali kuliko zahabu, inapaswa kupimwa kusudi ijulikane kuwa ya kweli. Na kwa sababu hii mutapata sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atakapotokea.


Kisha miti ikauambia muti wa tini: ‘Ukuje wewe utawale juu yetu.’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ