Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 2:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Siku moja, mutu wa Yawe alimwendea Eli, akamwambia: “Yawe amesema hivi: Nilijijulisha kwa jamaa ya Haruni, babu yako, walipokuwa watumwa wa mufalme wa Misri katika inchi ya Misri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 2:27
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku moja Yeroboamu alikuwa akisimama pembeni ya mazabahu kusudi afukize ubani. Basi, mutu wa Mungu kutoka Yuda akafika pale Beteli na ujumbe wa Yawe.


Basi, mufalme Solomono akamufukuza Abiatari, asikuwe kuhani wa Yawe. Hivyo likatimia neno alilosema Yawe kule Shilo, juu ya Eli na ukoo wake.


Yawe akamwambia Musa na Haruni, walipokuwa wangali katika inchi ya Misri:


Yawe akamwambia Musa na Haruni: “Haya ndiyo maagizo juu ya Pasaka. Mugeni yeyote hatashiriki chakula cha Pasaka.


Yawe akamwambia Haruni: “Kwenda katika jangwa ukutane na Musa.” Basi, Haruni akaenda, akakutana na Musa kwenye mulima wa Mungu, akamubusu.


Hii ndiyo baraka ambayo Musa, mutu wa Mungu aliwatakia Waisraeli mbele ya kufa kwake. Alisema hivi:


Lakini wewe mutu wa Mungu, uepuke mambo haya, ushikamane na haki, ibada, imani, upendo, uvumilivu na upole.


Maana hakuna hata ujumbe wowote uliotetewa kwa mapenzi ya kimutu, lakini watu walipasha ujumbe wa Mungu wakiongozwa na Roho Mutakatifu.


Mwanamuke huyo akaenda kumwambia mume wake: “Mutu wa Mungu ambaye sura yake ilikuwa kama ya malaika wa Mungu alinitokea. Sikumwuliza anatoka wapi wala hakuniambia jina lake.


Yawe akawapelekea nabii, naye akawaambia: “Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Niliwaondoa katika inchi ya Misri ambako mulikuwa watumwa,


Siku hiyo, nitatimiza yale yote niliyosema tangu mwanzo mpaka mwisho juu ya Eli na juu ya jamaa yake.


Wakawatafuta kwenye inchi ya milima ya Efuraimu na eneo la Shalisa, lakini hawakuwaona kule. Halafu wakafika Salimu, na kule hawakuwaona. Wakawatafuta katika inchi ya Benjamina, hata hivyo hawakuwapata.


Yule mutumishi akamwambia: “Ngoja kidogo. Katika muji huu kuna mutu wa Mungu ambaye anaheshimiwa sana. Kila neno analosema linakuwa kweli. Sasa tumwendee. Labda anaweza kutuambia jinsi safari yetu itakavyokuwa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ