Lakini Yehu hakutii sheria za Yawe, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuacha zambi zile za Yeroboamu ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi.
Lakini ninyi makuhani mumegeuka na kuacha njia ya haki. Mafundisho yenu yamewaongoza watu wengi katika kutenda mabaya. Mumelivunja agano nililofanya nanyi.
Kwa maana kwa masemi yao ya kujivuna na yasiyokuwa na maana, na kwa njia ya tamaa zao mbaya za kimwili, wanawavuta watu ambao wanaanza kuwaepuka, na wale wanaoishi katika udanganyifu.
Watu wote wameshuhudia Demetrio vizuri; hakika ukweli wenyewe unahakikisha jambo lile. Sisi vilevile tunamushuhudia, nawe unajua kwamba ushuhuda wetu ni wa kweli.
Lakini niko na neno hili juu yako: unamuvumilia yule mwanamuke Yezebeli, anayejiita kuwa nabii wa Mungu. Yeye anawapotosha watumishi wangu akiwafundisha kufanya uasherati na kula nyama za kutambikia sanamu za miungu.
Wakati ule, Eli alikuwa muzee sana. Aliposikia yote ambayo wana wake walikuwa wanawatendea Waisraeli, jinsi walivyokuwa wanalala na wanawake waliokuwa wanatumika kwenye mulango wa Hema ya Kusanyiko,