Mungu wangu, yule ambaye ninamukimbilia, ngao yangu, nguvu ya wokovu wangu, munara wangu, kimbilio langu. Mwokozi wangu, unaniokoa kutoka watesaji wakali!
akasema: “Ee Yawe, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu mwingine kama wewe, juu mbinguni, au chini katika dunia. Wewe unashika agano lako na kutenda wema kwa watumishi wako wanaoishi wakikutii kwa moyo wao wote.
“Ewe Yawe, ni nani kati ya miungu anayelingana nawe? Ni nani aliyekuwa kama wewe unayekuwa mutakatifu mukubwa, unayetisha kwa matendo matukufu, unayetenda mambo ya ajabu?
Enyi watu wangu, musiogope wala musikuwe na hofu, Sikuwaambia tangu zamani mambo yatakayotokea? Ninyi ni washuhuda wangu. Kuna mungu mwingine isipokuwa mimi? Kuna mwenye nguvu mwingine? Yule simujui!
Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.
Kwa sababu mimi ni Yawe, Mungu wenu, mujitakase na kuwa watakatifu kwa maana mimi ni mutakatifu. Wala musijichafue na kitu chochote kinachotambaa juu ya inchi.
Na yote yaliyoandikwa zamani katika Maandiko Matakatifu yameandikwa kwa ajili ya kutufundisha sisi, kusudi tuendelee kuchunga tumaini kwa njia ya kuvumilia na kufarijiwa sawa tunavyofundishwa katika Maandiko Matakatifu.
‘Ee Bwana wetu Yawe, ninajua umenionyesha mimi mutumishi wako mwanzo tu wa ukubwa wako na uwezo wako. Maana, kuna mungu gani huko mbinguni au katika dunia anayeweza kufanya mambo makubwa na ya ajabu kama vile ulivyofanya wewe?
Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.
Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.