Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 2:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Na kama mutu huyo akimujibu: “Ngojea kwanza niteketeze mafuta halafu utakamata kadiri unataka”, hapo huyo mutumishi wa kuhani anamujibu: “Hapana, unapaswa kunipatia sasa hivi. Kama sivyo, nitaitwaa kwa nguvu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 2:16
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watawala walionitangulia walikuwa muzigo muzito kwa watu wakiwadai chakula na divai. Zaidi ya hiyo waliwalipisha vikoroti makumi ine vya feza. Hata watumishi wao waliwatesa watu. Lakini, mimi sikufanya hivyo, maana nilimwogopa Mungu.


Kuhani ataviteketeza juu ya mazabahu kama chakula kinachotolewa kwa Yawe kwa moto kutoa harufu ya kumupendeza Mungu. Mafuta yote ni ya Yawe.


Yawe anasema hivi juu ya manabii wanaowapotosha watu wake, manabii ambao wanatabiri amani wakipewa kitu, lakini wanawatishia watu kwa vita wasipopewa kitu:


Watu wa kabila la Dani wakamwambia: “Afazali uache kelele zako, kama sivyo wengine wetu wenye hasira wanaweza kukushambulia, nawe utapoteza maisha yako na maisha ya jamaa yako.”


Zaidi ya hayo, hata mbele mafuta hayajateketezwa kwa moto, mutumishi wa kuhani anakuja na kumwambia yule mutu anayetolea sadaka: “Mumutoshee kuhani nyama ya kuchoma maana yeye hatapokea nyama yako iliyotokoteshwa, lakini inayokuwa mbichi.”


Zambi hii ya vijana hao wa Eli ilikuwa kubwa sana mbele ya Yawe. Maana, vijana hao walizarau matoleo ya Yawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ